Hadithi za gody daprince

Hadithi za gody daprince Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Hadithi za gody daprince, Book shop, Gody da prince@go. com, Dar es Salaam.

THE CREATURES(Mradi wa Siri)Ep.... 01Umri.... +18Mtunzi.....GODFREY P. EMMANUELYTungo: Nambari 7  Maktaba: 06/05/26mawas...
10/05/2026

THE CREATURES
(Mradi wa Siri)
Ep.... 01
Umri.... +18
Mtunzi.....GODFREY P. EMMANUELY
Tungo: Nambari 7
Maktaba: 06/05/26
mawasiliano... 0697704010


KATIKA SITU WA KOMANGAYA.

usiku wa manane mwaka 2001...

Msitu haukupumzika usiku ule.
Upepo ulipiga bila sababu. Ndege walinyamaza. Hata wadudu wale wanaolia kila usiku bila kukosa walinyamaza ghafla, kana kwamba asili yenyewe ilijua kilichokuwa kikitokea ndani ya msitu ule wa giza.

Mvua ilianza polepole. Tone moja. Mbili. Kisha kwa dakika chache ikageuka dhoruba...

mvua nzito iliyopiga majani kwa nguvu, ikafanya sauti ya vita ndogo ndogo kote msituni.

Radi ilipasua anga.
RRAAAH!

Mwanga wake mkali uliangazia kwa sekunde moja na katika mwanga huo, k**a picha ya ndoto mbaya, ilionekana banda la mbao lililosimama peke yake katikati ya msitu.

Banda zito. Banda la siri. Banda ambalo halikuwa kwenye ramani yoyote ya wilaya ile.

Ndani ya banda hilo
Kulikuwa na harufu ya damu na woga.

Wanawake saba wajawazito wamelala sakafuni juu ya magunia machafu. Mikono yao imefungwa minyororo iliyopigwa kwenye nguzo za mbao. Miguu yao vivyo hivyo. Hawakuweza kusogea. Hawakuweza kukimbia. Wangeweza tu kulala na kuomba.

Walikuwa wakilia.

Si kilio cha kelele. kilio cha kelele kilikwisha muda mrefu uliopita, usiku wa kwanza walipofika hapa, wiki tatu zilizopita.

Sasa walikuwa wakilia kwa kimya. machozi tu, bila sauti, k**a mto unaotiririka bila nguvu.

Mmoja wao mdogo kuliko wote, asiyeonekana na miaka zaidi ya ishirini alikuwa akisogeza mdomo wake bila sauti.

Alikuwa akisali. Sala yake ilikuwa rahisi. alikuwa akisali kuhusu usalama wake na mtoto aliye tumboni.

Mbele yao, alisimama mwanamume mmoja.
Alikuwa mrefu. Mwembamba kwa namna isiyo ya kawaida k**a mtu ambaye mwili wake ulifanya kazi moja tu na haukujali kitu kingine chochote. Alivaa joho jeusi lililomfikia visigino.

Usoni alikuwa na barakoa ya chuma iliyotengenezwa kwa makini. sehemu za uso zote zimefunikwa, macho tu yanayoonekana kupitia mashimo mawili meembamba.

Macho yake hayakuonyesha huruma.

Hayakuonyesha hasira pia.

Yalionyesha kitu kibaya zaidi... utulivu.

Utulivu wa mtu ambaye amefanya uamuzi wake muda mrefu uliopita na hakubali tena kuubadilisha.
Mkononi mwake alishika sindano kubwa ndefu k**a kalamu mbili zilizounganishwa.

Ndani ya sindano hiyo, kulikuwa na kioevu cheusi kilisogea polepole, kizito, k**a mafuta machafu yaliyochanganyika na kitu kingine kisichojulikana.

Akaitazama sindano kwa sekunde moja.
Kisha akawatazama wanawake.

"Usiku wa leo," alisema na sauti yake iliyofanana na chuma kinachogongana na chuma kingine.

"mtakufa nyote." alisema tena huyo mwanaume.

Mwanamke mmoja yule mzee zaidi, mwenye nywele za makaa akainua kichwa chake kwa nguvu zake zote zilizobaki.

"Tafadhali," akasema. Sauti yake ilikatika katikati.

"Daktari Kifo... muache mtoto wangu. Mimi sina hatia yoyote. Tulikuwa tu watu wa kawaida huko mtaani"

"watu wawaida?" Daktari Kifo akageuka kidogo. Kichwa chake kikainama upande mmoja k**a ndege anayesikiliza sauti ya mbali.

"Hakuna hata mmoja wenu aliyekuwa wa kawaida. Tangu mlipochaguliwa."
Akasogea mbele hatua moja ya polepole.

"Project Giza. Mnaikumbuka? Miaka mitano iliyopita sindano ile ndogo mliyopewa hospitali. Walikuambia ni chanjo. Walikuambia ni dawa ya malaria."
daktari kifo alisema mbele ya mwanamke yule mzee. Akaiinama kidogo akimwangalia kupitia mashimo ya barakoa yake.

"Ilikuwa damu. Damu ya simba. Nyoka. Popo. Na nyani. Imefichwa ndani ya mwili wenu kwa miaka mitano ikisubiri siku hii. Leo mtajifungua. Lakini hamtajifungua binadamu."

Ukimya mzito ukatua bΠ°ndani Kisha mwanamke mdogo yule aliyekuwa akisali akainua uso wake kwa mara ya kwanza. Macho yake yalikuwa mekundu ya machozi lakini ndani yake kulikuwa na kitu kingine. Moto mdogo wa hasira iliyofungwa.

"K**a utamuua mtoto wangu," akasema kwa sauti ya chini lakini thabiti, "nitakuapiza. Hata baada ya kufa β€” nitakufuata."

Daktari Kifo akamwangalia kwa muda.
Kisha kwa mara ya kwanza akatabasamu. Tabasamu ambalo halikuonekana chini ya barakoa yake, lakini lilionekana katika macho yake. Tabasamu baya.

"Hiyo ndiyo," akasema polepole,

"nilitarajia kusikia."
Akainua sindano.
CHWA!

Mwanamke wa kwanza alipiga yowe.

CHWA! CHWA! CHWA!

Mmoja baada ya mwingine walichomwa sindano.

Wanawake wakapiga kelele kali.
kelele zilizopanda juu ya mvua, juu ya radi, zikapotea msituni bila mtu yeyote kusikia.

Miili yao ilianza kubadilika polepole Kwa uchungu mkubwa. matumbo yakawavimba. si kwa njia ya kawaida ya kujifungua, bali kwa njia ya kitu kingine. kitu ambacho kilikuwa kikijaribu kutoka ndani kwa nguvu zake zote.

Mishipa ya shingo ikajitokeza. Macho yakabadilika rangi. ya kwanza yakawa ya njano, ya pili yakawa ya kijani, ya tatu yakawa nyekundu k**a damu.

Kucha zikaanza kukua ndefu, nyeusi, zenye makali. Meno yakatokeza k**a vile kinywa kilikuwa kidogo mno kuyashikilia.

Kisha Kimya kikatawala tena.

Kimya cha sekunde chache ambacho kilionekana k**a masaa.

WAAA! WAAA! WAAA!

Kilio cha watoto saba kikasikika kwa wakati mmoja. Lakini haikuwa kilio cha kawaida. Ilikuwa mchanganyiko. nusu kilio cha mtoto, nusu ngurumo ya kitu ambacho hakikuwa na jina.

Daktari Kifo akasimama wima.
Akatazama viumbe vipya vilivyokuwa vikilia mbele yake.

walikuwa watoto wadogo, wekundu, wenye nguvu tayari ambazo hazikuonekana kwa watoto wachanga wa kawaida.

Nyuma yao, wanawake saba walipumua mara ya mwisho. Mmoja mmoja Bila kelele K**a taa zinazozimwa na mkono usioonekana.

Daktari Kifo akapiga makofi polepole na kusema Kimya Kimya.

"Wamezaliwa, Namba moja mpaka saba. Watoto wa Giza hawa." alisema Akasimama pale kwa muda mrefu akiwatazama katika giza la banda, mvua ikiendelea kupiga nje, radi zikiangaza nyuso zao ndogo za ajabu.
Akafungua daftari lake jeusi. Akachukua kalamu.

Akaandika maneno majina saba.

Baraka. Zai. Winnie. Jini. Jocco. Sojjar. Pupwe.

Akafunga daftari..

"Miaka 25 Nitawasubiri. Na wakati utakapofika mtakuja wenyewe nyumbani." alisema daktari kifo.

ITAENDELEA

RICHMOND NA RAYMONDEp.........    07umri........ +18Mtunzi....... Godfrey P. Emmanuelytungo........ nambari 3maktaba.......
09/05/2026

RICHMOND NA RAYMOND
Ep......... 07
umri........ +18
Mtunzi....... Godfrey P. Emmanuely
tungo........ nambari 3
maktaba.... 8/5/24-
Simu......... 0697704010
Gmail........ [email protected]............................................................................................................ENDELEA.....................
"poa haina noma" mzee akaingiza mkono mfukoni akatoka na burungutu la hela, akalichambua na kumpatia roby elfu thelathini kisha wakaagana mzee akarudi ndani ya ukumbi nae roby akaelekea kwenye kituo cha daladala.

muvi iliendelea kuoneshwa hadi mida ya saa nne ikaisha. richimond na susumila wakatoka nje ya kumbi wakiwa wamejaa mashamsham. maneno mengi yalimtoka susumila wakati mwenzake akiisogelea pikipiki kubwa ijulikanayo k**a farasi mweupe, akapanda na kumsubiri susumila ajekupanda lakini susumila alikuwa kajisahau kabisa ndo kwanza ana hadithia kilichotokea katika muvi.

"susumila ni muda wa kurudi nyumbani sasa!" sura ya richimond ilinuna na sauti ya mamlaka ikamtoka kuonesha alikuwa bize na muda kwaiyo habari za maongezi mengi ya siyo maana hakuhitaji.

kwa vile binti susumila anamjua vema richimond ilibidi apande juu ya pikipiki kulikoni kuendeleza maongezi maana Richmond hakuhitaji story tena. aliwasha pikipiki wakaelekea maeneo ya baruti huko buguruni takasa.

walipokuwa wakienda hapakuwa mbali sana ila ilitosha kukaa juu ya pikipiki zaidi ya dakika kumi na mwisho pikipiki ikapaki nje ya nyumba kubwa inayo lindwa kwa geti la bati na sinyenge za draft.

"richi usiniambie na leo tena unaishia nje" alisema susumila baada ya kushuka kwenye pikipiki wakiwa wamesimama pembeni kidogo wamekumbatiana.

"ni kweli leo sitafika kwenu maana nina safari ya mbali kidogo na ni ya muhimu sana inatakiwa niende kwaiyo suala la mimi kuingia nyumbani kwenu tufanye siku nyengine"

"kwaiyo unataka kuniambia mimi na mama yangu hatuna umuhimu kwako?"

"hamna susu usiseme hivyo, nawapenda sana tu ila.."

"ila nini richi! mimi sitaki kusikia chochote zaidi ya kitendo cha wewe kuingia nyumbani kwetu na kukutana na mkwe wako. kwani tatizo nini wakati tayari mama anajua kila kitu na wewe si mgeni nyumbani kwetu, umekuwa ukija mara nyingi! sasa kwanini hivi karibuni umeianza tabia mpya ya kutohitaji kufika kwetu mpaka mama amekuwa akinisumbua kwa maswali ya kukuulizia wewe?" susumila aliongea kwa king'ong'o akajiegemeza kufuani mwa richi akizidi kumkumbatia kwa nguvu.
HADITHI HII INARUSHWA TOKEA PAGE YA GODFREY P. EMMANUELY, (utunzi ndio hajira yetu). UNAWEZA UKATUCHANGIA KWA KUSHARE HII HADITHI ILI IWAFIKIE WENGI ZAIDI.

PIA HII NI HADITHI TAMU KULIKO, KWAIYO UKICHELEWA KUPAKUWA VIPANDE NDIVYO UNAVYO BAKIWA NA UCHACHU MOYONI, HIVYO BASI, UNAWEZA UKALIPIA VIPANDE SITA KWA MIATANO, YAANI:

shilingi 500,
vipande 6

namba ni: 0697704010
jina ni: JOYCE J. MAGAJI

mtandao ni: Airtel

KARIBU......
"lakini susu.."

"hiyo lakini bado sitaki kuisikia!"

"ee ok, basi sawa nimekubali nitafika kwenu." mwisho richimond aliamua kukubali kuingia ndani kwa kina susumila. susumila akalisogelea geti la mabati akagonga hodi na muda si mrefu alikuja mama mmoja mwingi wa mwili na kufungua.

"hee jamani mwanangu richimond hupo wewe!?"

"ndio mama mimi nipo. sikamoo"

"malahaba.. ee yaani tangu nikuone siku hile ya happy birthday ndo mpaka leo sijakutia machoni, tatizo nini mpendwa au labda nimekukwaza sehemu ndio maana hautaki kufika hapa?"

"hapana mama usiseme hivyo, mbona mimi nipo na sina mpango wowote wa kuacha kufika hapa na wala haujawahi kunikwaza tena sifikirii kabisa k**a kunasiku utakuja kunikwaza, unanipenda sana mama." Richmond na mama susumila wakakumbatiana kwa muda kidogo kisha mama susumila akawataka waelekee ndani ya nyumba ambayo ilikuwa mita kadhaa toka getini.

haikuwa nyumba kubwa sana na wala haikuwa nyumba ndogo sana ilikuwa ya wastani yenye vyumba vitatu vya ndani.

"karibuni sana. susumila, mtake mwenzako mkae hapo" mama susumila aliyekuwa na furaha nyingi aliwapa maelekezo kuhusu sehemu nzuri ya kukaa.

"ahsante mama" richimond akaitikia kwa kushukuru huku ak**eti kochini.

"hivi hakuna juisi kwenye friji?" akauliza mama susumila naye susumila akamjibu kwamba hakuna juisi kwenye friji.

mama susumila akatoa noti ya shilingi elfu tano katika bindo la nguo ili susumila aende dukani akamfuatie mgeni soda lakini richimond aliipinga hatua hiyo akihitaji kujivika jukumu. ikawa mechi tafu wakati mama susumila akihitaji pesa yake itumike kununulia soda na richimond akitaka hela yake yeye ndo itumike kununulia soda mwisho richimond akaachiwa ajinafasi kwenye maamuzi yake.

"sasa wewe nisubiri hapa acha mimi nikafuate soda. ni hapo tu jirani muda si mrefu nitakuwa nimeredi" alisema susumila baada ya kupokea pesa akiwa wima tayari kwa ajili ya kwenda dukani lakini richimond alimtaka waende wote huko dukani.

"sasa si unisubiri tu hapa mimi nakuja sasaivi ya nini uanze kutahabika na utelezi wa balabala zetu chafu zilizolowana mvua na kuwa hazitamaniki??"

"wewe susu embu acha kujidanganya, ulishawahi kusikia wapi korosho inaweza kujishika bila ya bibo? hapo suala la kwenda dukani peke yako na kumuacha richimond hapa ni sawa na kupiga dufu la kula daku bila ya uwepo wa kinyago maana yeye ndio wewe na wewe ndio yeye... kivuli huvulika chini ya mshelisheli mwanangu!!" hapo wapenzi wawili walifurahi sana kwa kusikia kiswahili cha bi sikitu mwenye tanabari nyingi na methali zisizo idadika.

"mmh ila mama na wewe uhenga umekujaa mh!" susumila alifulahi sana kisha yeye na richimond wakatoka nje na kwenda lilipo duka.
HADITHI HII INARUSHWA TOKEA PAGE YA GODFREY P. EMMANUELY, (utunzi ndio hajira yetu). UNAWEZA UKATUCHANGIA KWA KUSHARE HII HADITHI ILI IWAFIKIE WENGI ZAIDI.

PIA HII NI HADITHI TAMU KULIKO, KWAIYO UKICHELEWA KUPAKUWA VIPANDE NDIVYO UNAVYO BAKIWA NA UCHACHU MOYONI, HIVYO BASI, UNAWEZA UKALIPIA VIPANDE SITA KWA MIATANO, YAANI:

shilingi 500,
vipande 6

namba ni: 0697704010
jina ni: JOYCE J. MAGAJI

mtandao ni: Airtel

KARIBU......
walifika dukani wakiwa na chupa tupu kwa ajili ya kubadirishana dhidi ya chupa zenye soda na walipo maliza kuhudumiwa wakarudi nyumbani wakaketi mezani wakijumuika na bi sikitu au mama susumila.

waliongea mengi sana wakacheka na kufurahi kisha richimond akaaga na kuondoka zake.

siku ilipita ikafuata nyengine. asubuhi ya saa mbili katika mitaa ya kanisani huko kinondoni b kuna mlango wa chumba ulifunguliwa na ndani akatoka kijana Robert akiwa na kinjunga ama kipande cha suruali huku kifua kikibaki wazi kwa kukosa shati wala fulana.

alifika nje akaelekea bafuni na kujisafisha kinywa akaoga kisha akarudi katika chumba cha pili tofauti na alichoamkia yeye na akagonga chumba hiko ndani ikasikika sauti ya k**e ikiitikia hodi.

"nani, robert?"

"ndio"

"enhee nini tena!?"

"za asubuhi mama"

"salama"

"shikamoo"

"marhaba"

"umeamkaje "

"salama"

"unaendeleaje"

"salama"

"unajisikiaje"

"eh we robert umevuta bangi nini?? salamu gani hiyo ya masaa, embu k**a hauna jipya kalale" mwana mama aliye kuwa ndani ambaye ndie mama wa robert alisitisha salamu ndefu k**a namba za nida inayotoka kwa mwanaye.

bi maria alimzoea sana mwanae kuwa ni mtu wa utani tangu utotoni mwake, hivyo kitendo cha yeye kusalimiwa salamu ndefu aliona ni kawaida na ni sehemu ya muendelezo juu ya ucheshi wa mwanae.

"sasa mama vipi kuhusu chai"

"lakini we mtoto mbona unavisa., unaniulizaje mimi masuala ya chai na unajua jiko lilipo" sauti ya mama Robert ilionesha fika upole wake na ilionesha jinsi alivyo chovuka asubuhi hiyo ila ndo hivyo tena, mama mpole lakini mtoto ni mchachu haswa! hawezi kukaa masaa mawili bila ya kumchalua mama yake endapo atakuwepo hapo nyumbani.

roby ni kijana mchangamfu na ana chembechembe za utundu alizotoka nazo utotoni na kuziamishia ujanani. kwa jinsi alivyo mwana harakati na mpirika pirika k**a wewe ni mmoja kati ya wale wasiopenda midhaa, basi usingeweza kukaa pamoja nae au hata kuongozana nae maana roby anapenda sana midhaa na hajuagi kununa hivyo k**a wewe ni mtu wakukaa kimya ama kwa lugha ya kimtaani tuna sema k**a wewe ni mtu wa kula bati basi haupaswi kujiunga na Robert mnaweza kurushiana mawe bure.

pamoja na kua maria amemzaa na kumlea lakini tabu aliipata kwani daima yeye ni mama mpole sana hapendagi kuongea bila ya msukumo, na hapendi sana midhaa lakini naweza kusema mtoto wake ndiye kiwanda cha midhaa, tena miongoni mwa watu anaopenda kuwatania ni mama yake. yaani hajisikii vizuri siku ikikatika bila yeye kumtania mama yake..

roby aliliendea jiko la kuni akavunja vijikuni vilivyokuwa ndani ya banda la jiko akaandaa sufulia la maji kisha akabandika chai..

kam hawa ndo huwa malast born
je, nini kitaendelea?

tukutane kwenye sehemu ya pili..

mimi mwandishi wako ni Godfrey P. Emmanuely.

ITAENDELEA

04/05/2026

mpoooo......?????

03/05/2026

asubuhi njema tokea mashariki mwa tanzania πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

soon
14/02/2026

soon

08/02/2026

The right email address for you βœ” Secure βœ” 100+ domain names βœ” Up to 10 mail addresses βœ” Sync across devices βœ” 65GB email storage βœ” Sign up today!

05/02/2026

With Dr William Mtanzania Wa USA America – I'm on a streak! I've been a top fan for 5 months in a row. πŸŽ‰

04/02/2026

"an'aa basi! basi! mwanangu, haupaswi kuwa na gazabu.. ngoja nimpigie....." alisema mzee akabonyeza simu yake kwa pupa na kumtafuta Joseph sindano.
"asa huyu naye sijui k**a atapokea simu maana yupo kanisani daa!.." aliongea mzee huku akikuna kichwa kwa mawazo msongo. bahati nzuri simu ikapokelewa upande wa pili.
"ee halo Joseph, eee fanya haraka, chukuwa gari njoo hapa... hapaaa... maeneo yaa.. yaaa...." mara simu ya mchungaji ikaporwa. Henry Jeremiah aliona mambo yanakuwa mengi, mzee anashindwa kujieleza hivyo ikabidi ashike yeye simu.
"Joseph acha kunata, fanya haraka njoo kwenye kona ya edexi mparilo uingie pale kwenye kibanda cha simu ukasimame kwenye mgahawa wa magic flower. ukifika hapo upaki gari na uiweke standby kwa ajili ya kuwatorosha hawa uwapeleke kanisani kuna tatizo kidogo limetokea.... hey! nakupa dakika kumi!" Henry alimaliza kuogea na simu akairejesha kwa pastor kisha akapandisha na kushusha pumzi alafu akashika gia na kuinyonga vilivyo ili kuukoza mwendo. gari ilishika kasi kikawa inaiacha mbali ile gari nyeusi iliyo kuwa nyuma ila muda si mrefu na yenyewe ilikoza mwendo.... sasa ilikuwa ni dhahiri kuwa pastor na familia yake wanawindwa. kumbe ni kweli ile gari iliyokuwa nyuma yao haikuwa gari sahihi kutokana na watu waliyokuwa wakiiendesha. watu waliyo kuwa kwenye gari ya nyuma walikuwa na mpango wa kumuua pastor. ni wauwaji ambao hawajulikani wametumwa na nani... bado haijajulikana kisa cha kufuatiliwa kwa pasta ila msako ulikuwa mkali. wavamizi walimsaka pastor kwa udi na uvumba na leo jaribio lao la pili linakwenda kuchachafya nyoyo za watu... kufa ama kupona ndio hatua iliyo baki mbele ya macho ya kila mmoja....
UPANDE WA PILI....
kijana mmoja mwembamba mrefu mweusi alitoka kanisani na kuitazama gari nyeupe iliyo hatua 13 toka kwenye sakafu ya kanisa.
✍️
"josee.." sauti nyembamba ya k**e ililitaja jina la handsome boy wakanisa la kiangarikana. nyuma ya mgongo wa Joseph alisimama nusu malaika mmoja mwenye rangi ya mtume.
"evah" joseph aliitika kwa kulitaja jina la mlimbwede aliye nyuma yake bila ya kumtazama. alimtambua kwa kupitia sauti.
"unakwenda wapi na ibada ipo karibuni kuanza?"
"kuna mtu nakwenda kumfuata"
"nani? mchungaji?"
"hapana, mchungaji anakuja na Henry"
"vipi tunaweza kwenda wote?"
"hapana ni private kidogo"
"jamani joseph ndo umesha fikia huko!!? unani bakisha k**a mtu baki..."
"evah haupaswi kulalamika, unatakiwa kwenda ibadani" alisema jose akimalizia kufunga mlango baada ya kuingia ndani. haraka aliwasha gari na kutoweka maeneo hayo huku mrembo evah akibaki kumtazama kwa kiu. nidhahiri kuwa evah alikuwa anampenda sana kijana joseph na kila afumbapo macho yake alikuwa akiiona ndoa yao ikifungwa kwenye kumbi ghari sana. nifikra tu ila kiuhalisia kanisani. mapenzi hawana mausiano ya karibu ushirika wayanaumiza mapenzi yanatesa mapenzi yanauwa. kupenda sio ujinga wala uzembe ila ukipenda pasipo na ujari ni mateso. chozi la church girl lilidondoka kwamatone ya awamu. macho yake yakapoteza langi nyeupe nagavu nakuwa mekundu kasoro. hakuna alicho kifanya zaidi ya kufuta machozi kwa kitambaa cha leso na kurudi ndani ya kanisa huku miyo wake ukisukuma damu kwa shida baada ya kukosa nafasi ya kutulia pamoja na mtu ampendae.
mtaalamu joseph sindano chapu aliingizia garini barabara kuu na kuelekea maeneo ya sudika. wakati akiwa njiani simu yake iliita akaipokea na kuiweka sikioni.
"sindano, ukowapi?"
"nipo kwene barabara ya tatu nakaribia eneo la tukio"
"akikisha unawahi kufika kabla ya dakika sab tupo karibuni kufika ina takiwa uwe umwtangulia" alisema Henry huku akiongeza speed ya gari kuwakwepa .ajangiri wanao kuja nyuma yao. ambao walikuwa wakiongeza kasi kila baada ya mda mchache. uzuri ni kukwa Henry Jeremiah alikuwa mtaalamu wa kukimbiza gari.
muda dakika kumi natano ulitosha kuifikisha gari aina toyota VIP nesma TVN 331 nje ya mgahawa wa MAGIC FLOWER. kijana Joseph sindano alishuka na suti yake nyeupe akaangaza mazingira na kufungua mlango mkubwa wa gari akauacha ivyoivyo (wazi).
"karibu kaka" sauti itizi ilipiga mbizi kwenye masikio yake ufahamu ukamfahamisha kuwa duniani kuna mauwa nq ndege waimbao sauti nzuri. sauti iliyo muita hapo ilikuwa ni sauti tekenyi inayo tekenyua hisia. alimtazama huyo mwanamke kisha akaregesha macho garini kuanga k**a kila kitu kipo sawa.
"mna sambusa za kiazi kitamu?"
"ndio zipu, karibu. pita ndani"
"hapa niletee sambusa tatu nakula hapa hapa nje" maagaizo yalikuwa ni hayo na kwakuwa mteja ni malmyibidi tu iwe hivyo japo wafanya biashay wa huo mgahawa walitamani apite ndani. joseph alisubiri sambusa za viazi vitamu huku akiwa standby kushuhudua tukio jipya.
"sambusa hizi hapa, ngoja nikuletee kiti"
"usiwaze kuhusu kiti, nitasimama hivi hivi" kijana joseph sindani hakuwa na mambo mengi alimtaka binti akaendeleze huduma kwa wateja wengine kwani yeye anaweza kula hivyo hivyo akiwa wima. wakati kijana Joseph sindano akiendea kutafuna sambusa mara gari nyeusi iendayo kasi ilifika ikatimua vumbi jingi kwa brake za ghafla. haraka! wakashuka watu wanne na kuzunguka nyuma ya gari aliyokuja nayo kijana Joseph sindano kisha gari hiyo gari nyeusi ikaendelea kuchapa mwendo. ilikuwa kitendo cha haraka kiasi kwamba mtu aliye chelewa kutazama asingejua kuna watu wanne wameshushwa. hapo hapo gari nyengine ilitokea nyuma ilikiwa bize ikapita wima na kuacha vumbi zito kweli kweli.
"we dada!" aliita joseph sindano akimuhita muhudumu nakumkabizi pesa zaidi ya themani ya sambusa alizokula. aliamini angesubiri zaidi ingekuwa hatari kwake na kwafamilia nzima ya pastor.
"Joseph! tuondoke bwana!" alima pastor kwa sauyi kali akiona kuchelewa. imani ilikuwa imemuenda rikizo. kijana joseph sindano.hakuwa na nafasi ya kukaidi maagizo zaidi ya kukaa vyema uskanini na kuondosha gari.
UPENDE MWENGINE:
gari mbili... ziliendelea kufukuzana kwa kasi sana zikipita vibonde vibonde vidogo vidogo maana ilikuwa laffrod. baadae gali yambele ikakunja kushoto.na kusimama.
pleee.....!!! muda mfupi gari nyengine ilikuja mbio ikakunja na kuseleleza.matailri ikapiga msele kwambele kisha waru watatu wakashuka chap! wakiwa na silaha za moto.mikononi. walikuwa wakimuhitaji pastor na familia yake kiujumla. kwa jinsi walivyo bana tairi za mbele haikuwa lahisi mlengwa wao kuwapotea. nilazima kwangewatia mikononi , hii ni kwamujibu wa mawazi ya. japo walikuwa na silaha za moto mikononi lakini hawakuwa na amani ya moja kwa moja, waliamini mpka gari imeegeshwa ghafla hivyo kutakuwa na mtego umeandaliwa juu yao hivyo wakawa wananyata pole! pole! walisogea mpaka katika gari wakafungua milango nakunyoosha midomo yabuduki.zao.sambba na kutayalisha vidore vyao kwa ajili ya kumteketeza myu yeyotealiye ndani yagari.
UPANDE A....
"baba, mko salama?" aliuliza Joseph sindano akik**atabmikanda ya gari na kuipachika mabegani kisha kufunga loc.
"tupo salama, ongza mwendo" alijibu pastor akionesha hofu iliyo.ndani yake. muda wote alikuwa bize kutazama kwenye vioo. hakuamini kwba bado yupo.salama mpaka muda huo.
"Joseph embu niambieni wale ni wakina nani?" mke wa mchungaji aliuliza kwa hofu na wasiwasi.
"mama alia haunahaja ya kuweweseka. wale ni watu wakawaida tu" akadakia pastor akimficha mkewe asitajue mengi ya kutisha. kijana agano alikaa vizuri kusukanini na sasa alikuwa tayari kuongeza mwendo. zaidi. kabla ya kuruhusu gia mpya alitazama nyuma wataka wafunge mikanda vizuri kisha safari ikaiva... haikujulikana wanakwenda wapi kwa.muda huo ila kuwa salama lilikuwa jambo jema zaidi ya yote....
UPANDE B
wavamizi walikuwa tayari kushoot ila hawakkuta mti yeyote ndani ya gari.. waliishiwa pizi mzee. wakati huo kijana Henry jeriah alikuwa amejibanza nyuma ya kichaka anasikilizia. kumbe alupo funga brake tu alitoka nje ya gari na kwenda kujificha nyuma ya kichaka...swap!.... mara kisu kizito kilipenya nyuma ya mvamizi mmoja. hapo kijana Henry jeriah ikuwa kashajifichua na kuja kuruka teke zito kwenye mgongo wa mvamizi ambaye nyuma yake kulikuwa na kisu kime zama k**a ichi mbili na nusu kilichorushwa na Henry... sasa kisu kilikandamizwa kikaingia ndani zaidi mbaka kikabakia mpini mtupu...
"aaaaa.....h!!!!" mvamizi aliye pigwa kisu alitoa yowe refuu kwa maumivu makali aliyoyapata. haraka kisu kikachumolewa mgongoni mwake. Henry hakuwapa nafasi.yz kufyatua risasi kwani alikuwa karibi na vifua vyao..pa!.. nafasi moja hafifu iliyo patikana ndio.iliyo fanya lisasi ichomoke na kupotelea hewani nila.ya malengo. hapo ngumi.nzito zili piga kwemye tumbo gumu la mvamizi kishab wide jeb yenye kilo 20 ilihusika kumuangisha k.o... mwengine anakuja nyuma yangongo wakijana Henry jeriah aliotewa heroes kick ya maana ikatua kwenye kijiji chasiri na kupasua magoroli mawili yanayo patikana huku..........whatassp 0783483825

ASUBUHI,nje ya fensi ya mabua.Mzee wa busara akiwa amesimama chini ya mti mkubwa wa mkuyu kwa ajili ya kupiga mswaki, ma...
27/01/2026

ASUBUHI,
nje ya fensi ya mabua.
Mzee wa busara akiwa amesimama chini ya mti mkubwa wa mkuyu kwa ajili ya kupiga mswaki, mara alidondokewa na tone la maji katika paji la uso wake.
kwa haraka hii hali ilimfikirisha kwa undani zaidi. Inakuwaje adondokewe na tone la maji nyakati za kiangazi bila ya mvua wala umande. Ndipo mzee wabusara alipoinua shingo yake kuangalia juu ya huo mti wa mkuyu. Alishangaa kumuona kunguru mmoja akiwa pekeyake tawini akilia kwa uchungu na majonzi tele. Hapo mzee wabusara alishusha mswaki wake wa mti uliyokuwa mdomoni kisha akamkazia macho yule kunguru na kumwambia, "ewee muwanda porini na mijini, ni nini kinakuliza?? Embu shuka chini unieleze shida yako. kunguru kwa kusikia sauti ya mzee wabusara iliyobeba mamraka ndani yake ilibidi ashuke kiunyonge na kutuwa begani mwa huyo mzee aliyeamua kijitenga pembezoni mwa kijiji cha pilipanda.
Ofkoz mzee wa busara ni mzee mwenye hekima kubwa katika huu ulimwengu wa dunia. Mzee wa busara alikuwa na uwezo mkubwa sana katika imani kiasi kwamba alikuwa hadi na uwezo kuongea na ndege pamoja na wanyama. HUKUMBELE MPENDWA MSOMAJI UTAKWENDA KUMFAHAMU VYEMA HUYU MZEE ILA KWA SASA TUENDELEE NA STORY.
"Niambie unalia nini ewe mja wa mungu usiye na hatia?" aliuliza tena mzee wabusara huku akiwa makini kusikiliza anachoongea kunguru. kunguru akajibu kiunyonge. Kunguru alisema hivi...
"Mzee wabusara, kwa kweli nimeyachoka haya maisha ya kutangatanga huku na huku kila siku, na mimi natamani kuishi k**a wanavyoishi kasuku" baada ya kunguru kusema hivyo mzee wabusara akacheka tena na kusema kwa sauti ya taratibu iliyobeba msisitizo.
"Ama hakika waja wa muumbwa wanaangamia kwa kukosa kujua haja ya mja..." kabla ya kuendelea mzee wabusara alikohoa kidogo Kisha akajiweka sawa na kuendelea.. "kunguru kwanza napenda utambue kuwa hata kobe hafurahishwi na gome lake. Sio kobe tu, hata twiga naye hafurahishwi na urefu wake... Je uliwahi kulijua hilo?? Je, umewahi kujua kuwa hata huyo kasuku afurahishwi na maisha yake?" Hapo kunguru akaguna baada ya kusikia hayo maswali ya mfurulizo yaliyo beba ukweli ndani yake hivyo ikabidi aulize swali jengine. "Sasa kwanini kasuku ayachukie maisha yake wakati ni mazuri sana??? Kasuku anafungwa kwenye sehemu nzuri iliyo tulia, kasuku anahudumiwa kwa kila jambo na mfugajiwake. kasuku analindwa na kutunzwa k**a lulu, kasuku anapendwa mpaka na watoto wadogo.. lakini mimi maisha yangu najitafutia mwenyewe chakula.. isitoshe binadamu wakiniona wananirushia mawe bila ya makosa, yaani maisha yangu yamekuwa ya kutangatanga bila ya amani na sijui mwisho wake lini." Mzee wabusara alimsikiliza sana kunguru kisha akamtazama kwa huruma na kumjibu kwa busara,
"Umeelezea vizuri sana kunguru lakini kuna vitu umevisahau. Umeshau kuwa kasuku haishi kwa uhuru k**a wewe. Kasuku anafungiwa kwenye banda kutwa kucha. Kasuku huwa hachagui ale nini, bali anachaguliwa na mfugaji wake. Muda mwengine kasuku hulazimika kula chakula asichokipenda kwa kukosa uhuru wa kwenda kujitafutia. Kumbuka kuwa kasuku anambawa zakuruka na kwenda mbali lakini ana uho uhuru, yeye ni wa bandani tu maisha yake yote! Je, ipi ni amani ya kweli, kuishi wanavyotaka ikiwa wewe hautaki ama kuishi unavyotaka ikiwa wao hawataki????" Swali la mzee wabusara lilimuacha kunguru kinywa wazi akabaki anajiuliza maswali kedekede ndani ya ya ubongo wake. Kwa mbali alianza kupata picha yakuwa bora yeye kuliko maisha ya kasuku...
MPENDWA MSOMAJI HILI SWALI ALILOULIZWA KUNGURU NA MZEE WA BUSARA. SWALI HILI LINAMAANA KUBWA SANA. UKWELI NI KWAMBA HATA SISI BINADAMU TUNAISHI NDANI YA HIZO TAMAA. YAANI MTU ANATAMANI KUWA K**A MTU MWENGINE BILA YA KUJUA MADHARA YAKE. KATIKA HII HADITHI UTAJIFUNZA MENGI SANA KUHUSU HILI SWALI AU JIBU LA MZEEE WABUSARA.
NIKUTAKE TU MPENDWA MSOMAJI USOGEE PEJINI NA UJISOMEE MENGI ZAIDI. NI MIMI MWANDISHI WAKO (BEKA KITATA).
HADI WAKATI MWENGINE... TUKUTANE KWENYE KIPANDE CHA PILI
AHSANTE..
itaendelea...

"an'aa basi! basi! mwanangu, haupaswi kuwa na gazabu.. ngoja nimpigie....." alisema mzee akabonyeza simu yake kwa pupa n...
19/01/2026

"an'aa basi! basi! mwanangu, haupaswi kuwa na gazabu.. ngoja nimpigie....." alisema mzee akabonyeza simu yake kwa pupa na kumtafuta Joseph sindano.

"asa huyu naye sijui k**a atapokea simu maana yupo kanisani daa!.." aliongea mzee huku akikuna kichwa kwa mawazo msongo. bahati nzuri simu ikapokelewa upande wa pili.

"ee halo Joseph, eee fanya haraka, chukuwa gari njoo hapa... hapaaa... maeneo yaa.. yaaa...." mara simu ya mchungaji ikaporwa. Henry Jeremiah aliona mambo yanakuwa mengi, mzee anashindwa kujieleza hivyo ikabidi ashike yeye simu.

"Joseph acha kunata, fanya haraka njoo kwenye kona ya edexi mparilo uingie pale kwenye kibanda cha simu ukasimame kwenye mgahawa wa magic flower. ukifika hapo upaki gari na uiweke standby kwa ajili ya kuwatorosha hawa uwapeleke kanisani kuna tatizo kidogo limetokea.... hey! nakupa dakika kumi!" Henry alimaliza kuogea na simu akairejesha kwa pastor kisha akapandisha na kushusha pumzi alafu akashika gia na kuinyonga vilivyo ili kuukoza mwendo. gari ilishika kasi kikawa inaiacha mbali ile gari nyeusi iliyo kuwa nyuma ila muda si mrefu na yenyewe ilikoza mwendo.... sasa ilikuwa ni dhahiri kuwa pastor na familia yake wanawindwa. kumbe ni kweli ile gari iliyokuwa nyuma yao haikuwa gari sahihi kutokana na watu waliyokuwa wakiiendesha. watu waliyo kuwa kwenye gari ya nyuma walikuwa na mpango wa kumuua pastor. ni wauwaji ambao hawajulikani wametumwa na nani... bado haijajulikana kisa cha kufuatiliwa kwa pasta ila msako ulikuwa mkali. wavamizi walimsaka pastor kwa udi na uvumba na leo jaribio lao la pili linakwenda kuchachafya nyoyo za watu... kufa ama kupona ndio hatua iliyo baki mbele ya macho ya kila mmoja....

UPANDE WA PILI....

kijana mmoja mwembamba mrefu mweusi alitoka kanisani na kuitazama gari nyeupe iliyo hatua 13 toka kwenye sakafu ya kanisa.

✍️

"josee.." sauti nyembamba ya k**e ililitaja jina la handsome boy wakanisa la kiangarikana. nyuma ya mgongo wa Joseph alisimama nusu malaika mmoja mwenye rangi ya mtume.

"evah" joseph

Address

Gody Da Prince@go. Com
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi za gody daprince posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category