Maju global products

Maju global products Tunajivunia kuuza Bidhaa Bora kabisa kwa kuwapelekea wateja mahali walipo (Dar es Salaam):-

•Mche

SHULE YA HUDUMA (NAMNA YA KUPONYA WAGONJWA) 18.09.2024
18/09/2024

SHULE YA HUDUMA (NAMNA YA KUPONYA WAGONJWA) 18.09.2024

KUNA MAMBO 7 NINGEKUSHAURI UYATAFUTE SANA K**A UNATAKA KUWA MTU KATI YA WATU HAPA DUNIANI1. UTAKATIFU (HOLINESS)Waebrani...
09/09/2024

KUNA MAMBO 7 NINGEKUSHAURI UYATAFUTE SANA K**A UNATAKA KUWA MTU KATI YA WATU HAPA DUNIANI

1. UTAKATIFU (HOLINESS)

Waebrania 12:14
[14]Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
Follow peace with all men, and holiness, without which no man shall see the Lord:

2. HEKIMA MBALIMBALI ZA MUNGU (DIFFERENT KIND OF DIVINE WISDOMS)

1 Wafalme 10:4-14
[4]Naye malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani, na nyumba aliyokuwa ameijenga,
And when the queen of Sheba had seen all Solomon's wisdom, and the house that he had built,
[5]na chakula cha mezani pake, na watumishi wake walivyokaa, na kusimamia kwao wangoje wake, na mavazi yao, na wanyweshaji wake, na daraja yake ya kupandia mpaka nyumba ya BWANA, roho yake ilizimia.
And the meat of his table, and the sitting of his servants, and the attendance of his ministers, and their apparel, and his cupbearers, and his ascent by which he went up unto the house of the LORD; there was no more spirit in her.
[6]Akamwambia mfalme, Ndizo kweli habari zile nilizozisikia katika nchi yangu za mambo yako na za hekima yako.
And she said to the king, It was a true report that I heard in mine own land of thy acts and of thy wisdom.
[7]Lakini mimi sikuzisadiki habari hizo, hata nilipokuja na kuona kwa macho yangu; tena, tazama, sikuambiwa nusu; wewe umezidi kwa hekima na kufanikiwa kuliko habari nilizozisikia.
Howbeit I believed not the words, until I came, and mine eyes had seen it: and, behold, the half was not told me: thy wisdom and prosperity exceedeth the fame which I heard.
[8]Heri watu wako, na heri watumishi hawa wako, wasimamao mbele yako siku zote, wakisikia hekima yako.
Happy are thy men, happy are these thy servants, which stand continually before thee, and that hear thy wisdom.
[9]Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti cha enzi cha Israeli; kwa kuwa BWANA amewapenda Israeli milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme, ufanye hukumu na haki.
Blessed be the LORD thy God, which delighted in thee, to set thee on the throne of Israel: because the LORD loved Israel for ever, therefore made he thee king, to do judgment and justice.
[10]Basi akampa mfalme talanta za dhahabu mia na ishirini, na manukato mengi, mengi sana, na vito vya thamani; wala haukuja tena wingi wa manukato, k**a hayo malkia wa Sheba aliyompa mfalme Sulemani.
And she gave the king an hundred and twenty talents of gold, and of spices very great store, and precious stones: there came no more such abundance of spices as these which the queen of Sheba gave to king Solomon.
[11]Tena merikebu za Hiramu, zilizochukua dhahabu kutoka Ofiri, zikaleta kutoka Ofiri miti ya msandali mingi sana, na vito vya thamani.
And the navy also of Hiram, that brought gold from Ophir, brought in from Ophir great plenty of almug trees, and precious stones.
[12]Mfalme akafanya kwa mia hiyo ya msandali nguzo za nyumba ya BWANA, na za nyumba ya mfalme, na vinubi na vinanda vya hao waimbaji; wala haikuja miti ya msandali k**a hiyo, wala haikuonekana, hata leo.
And the king made of the almug trees pillars for the house of the LORD, and for the king's house, harps also and psalteries for singers: there came no such almug trees, nor were seen unto this day.
[13]Naye mfalme Sulemani akampa malkia wa Sheba haja yake yote, kila alilotaka, zaidi ya hayo aliyopewa na Sulemani kwa ukarimu wake wa kifalme. Basi, akarudi akaenda zake katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And king Solomon gave unto the queen of Sheba all her desire, whatsoever she asked, beside that which Solomon gave her of his royal bounty. So she turned and went to her own country, she and her servants.
[14]Basi uzani wa dhahabu iliyomfikia Sulemani mwaka mmoja, ndio talanta mia sita sitini na sita,
Now the weight of gold that came to Solomon in one year was six hundred threescore and six talents of gold,

3. AINA MBALIMBALI ZA UPAKO (ANOINTINGS)

Hakuna aina moja ya upako, kuna pako mbalimbali, na ili uwe na matokeo kila mahali, tafuta hizo!

Luka 4:14
[14]Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.
And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee: and there went out a fame of him through all the region round about.

Matendo ya Mitume 10:38
[38]habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.
How God anointed Jesus of Nazareth with the Holy Ghost and with power: who went about doing good, and healing all that were oppressed of the devil; for God was with him.

Zaburi 23:5
[5]Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.
Thou preparest a table before me in the presence of mine enemies: thou anointest my head with oil; my cup runneth over.

4. NEEMA MBALI MBALI ZA MUNGU NA WALIZOBEBA WATU FULANI HAPA DUNIANI (GRACES OF GOD AND UPON MEN)

1 Petro 4:10
[10]kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; k**a mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
As every man hath received the gift, even so minister the same one to another, as good stewards of the manifold grace of God.

1 Wakorintho 15:9-10
[9]Maana mimi ni mdogo katika mitume, nisiyestahili kuitwa mitume, kwa sababu naliliudhi Kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, that am not meet to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
[10]Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am: and his grace which was bestowed upon me was not in vain; but I laboured more abundantly than they all: yet not I, but the grace of God which was with me.

5. MAARIFA KWENYE KILA ENEO LA MAISHA (KNOWLEDGE OVER EVERY SPHERE OF LIFE ESPECIALLY ON YOUR GOD GIVEN PURPOSE)

Isaya 5:13
[13]Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
Therefore my people are gone into captivity, because they have no knowledge: and their honourable men are famished, and their multitude dried up with thirst.

Mithali 24:5
[5]Mtu mwenye hekima ana nguvu;
Naam, mtu wa maarifa huongeza uwezo;
A wise man is strong; yea, a man of knowledge increaseth strength.

6. AKILI YA KUJUA NYAKATI NA MAJIRA NA NINI CHA KUFANYA KILA WAKATI AU KILA MAJIRA (UNDERSTANDING OF TIMES AND WHAT TO DO IN SEASONS)

1 Mambo ya Nyakati 12:32
[32]Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
And of the children of Issachar, which were men that had understanding of the times, to know what Israel ought to do; the heads of them were two hundred; and all their brethren were at their commandment.

7. HEKIMA NA AKILI YA KUHUSIANA NA WATU WA NAMNA ZOTE (WISDOM ON HOW TO LIVE WITH ALL MEN)

Mithali 14:28
[28]Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;
Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.
In the multitude of people is the king's honour: but in the want of people is the destruction of the prince.

Isaya 43:4
[4]Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.
Since thou wast precious in my sight, thou hast been honourable, and I have loved thee: therefore will I give men for thee, and people for thy life.

Luka 6:38
[38]Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Give, and it shall be given unto you; good measure, pressed down, and shaken together, and running over, shall men give into your bosom. For with the same measure that ye mete withal it shall be measured to you again.

HAYA YAKIWA MAISHANI MWAKO,
MAISHA UMEYAPATIA,
NA HAUTATUMIA NGUVU KUFANIKIWA,
YATAFUTE MPAKA YAWE MIKONONI MWAKO,

Pastor Dickson Cornel Kabigumila
Mchungaji Kiongozi ABC GLOBAL DUNIANI,
09/09/2022

THE RISING OF NATIONAL SOLUTIONS
01/06/2024

THE RISING OF NATIONAL SOLUTIONS

Ungana nami kwenye kipindi cha maisha ya kusudi siku ya kesho ambapo nimefanya mahojiano  na Pastor Sarah Kulindwa kuhus...
27/05/2024

Ungana nami kwenye kipindi cha maisha ya kusudi siku ya kesho ambapo nimefanya mahojiano na Pastor Sarah Kulindwa kuhusu wanawake na utumishi wa madhabahuni.
Tutakuwa live kwenye YouTube,Usikose tafadhali na waambie uwapendao pia. Link ya channel ya YouTube ya Maisha ya Kusudi hii hapa:

https://www.youtube.com/

Our Dear Pastor We appreciate your faithfulness and wish you the very best of birthdays. Happy Birthday Pastor Jordan Yu...
24/05/2024

Our Dear Pastor We appreciate your faithfulness and wish you the very best of birthdays.

Happy Birthday Pastor Jordan Yusuph

https://youtube.com/?si=BWP5rocVKXBghCsRTAFADHALI SUBSCRIBE SASA YOUTUBE YETU YA ABC GLOBAL MUDA MCHACHE KUTOKA SASA TUT...
17/05/2024

https://youtube.com/?si=BWP5rocVKXBghCsR

TAFADHALI SUBSCRIBE SASA YOUTUBE YETU YA ABC GLOBAL MUDA MCHACHE KUTOKA SASA TUTAKUWA LIVE KWENYE ACCOUNT HII (THE NIGHT OF ENCOUNTER -MBEYA) NA SHARE KWA WENGINE

JIFUNZE KUPITIA HEKIMA HIZI NA BISHOP DICKSON KABIGUMILA
26/04/2024

JIFUNZE KUPITIA HEKIMA HIZI
NA BISHOP DICKSON KABIGUMILA

DESTINY SHAPING GATHERING DAR ES SALAAM || Zakayo Nzogere || 23.03.2024
23/03/2024

DESTINY SHAPING GATHERING DAR ES SALAAM || Zakayo Nzogere || 23.03.2024

SEMINA YA UCHUMI NA FEDHA | ABC GLOBAL MWANZA DAY 2 | 12.12.2023
12/12/2023

SEMINA YA UCHUMI NA FEDHA | ABC GLOBAL MWANZA DAY 2 | 12.12.2023

K**a una mwanao, mdogo wako, ndugu yako, mwanachuo mwenzio aliye DIT, MUHAS, IFM, Mwalimu Nyerere (MNMA), DUCE, TIA, DIP...
13/11/2023

K**a una mwanao, mdogo wako, ndugu yako, mwanachuo mwenzio aliye DIT, MUHAS, IFM, Mwalimu Nyerere (MNMA), DUCE, TIA, DIPLOMASIA, BANDARI tusaidie kuwajulisha kwamba tuna KANISA MAALUM LA WANAVYUO WA VYUO HIVYO TAJWA HAPO JUU lililopo VIWANJA VYA MAONESHO VYA SABASABA katika HEMA YA MIKUMI...

JUMAPILI HII YA 19.11.2023 TUTASHUGHULIKIA VIZUIZI VYA HATMA VILIVYOKO VYUONI

KWENYE KIZAZI HIKI CHA SASA USIAMINI MWANAO, NDUGUYO AU MDOGO WAKO YUKO SALAMA CHUONI KWA SABABU AMETOKEA FAMILIA YA KIKRISTO AU AMEOKOKA TU, ANAHITAJI MALEZI, UANGALIZI NA USIMAMIZI ILI AWE BORA KIELIMU, KIROHO NA AANDALIWE KUWA JIBU LA TAIFA KWA MAFUNDISHO TULIYOANDAA KWA UTULIVU NA UMAKINI MKUBWA KWA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU...

MAWASILIANO
0753 466675
0655 466 675

ASSEMBLY OF BELIEVERS CHURCH KAHAMA.SIKU 8 ZA SEMINA YA UCHUMI.SIKU 6/8, MORNING GLORYNAFASI YA MSHIRIKA MMOJAMMOJA KATI...
06/10/2023

ASSEMBLY OF BELIEVERS CHURCH KAHAMA.
SIKU 8 ZA SEMINA YA UCHUMI.
SIKU 6/8, MORNING GLORY
NAFASI YA MSHIRIKA MMOJAMMOJA KATIKA UKUAJI WA KANISA
MH: ASK Dickson Cornel Kabigumila
06-10-2023.

Wajibu wa mshirika, mwendelezo:
5. Kuamua na kudhamiria kwa dhati kuwa barua ya Kristo kwa wenzio walio kanisani na waliokok nje ya kanisa.
Mathayo 5:13-16
"Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni."

Biblia inatufananisha na bidhaa 2 ambazo zinahitajika kila mahali.
1.Nuru
Hakuna mahali ambapo nuru haihitajiki.
2. Chumvi.

Kazi ya nuru ni kuwasaidia wengine kuona pale ambapo wasingeona. Dunia yote ina giza, na watenda dhambi wote wamefunikwa na giza.

2Korintho 4:3-4
"Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu."

Watu wanona nuru wanapomuona mkristo annaishi ukristo wanavutiwa na nuru yake.
Kadri mtu anavyoishi maisha ya nuru unasaidia dunia kuona usahihi.

1Petro 3:1-7
Wanawake wana nafasi kubwa kwenye kuleta watu kwa Yesu. Kazi yao kubwa ni kusambaza habari. Kanisa lolote ili likue lazima wanawake wajue nafasi yao katika kuwaleta wengine kwa Yesu. Kanisa lenye wanaume wengi kuliko wanaume haliwezi kukua.

"Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. K**a vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote. Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, k**a chombo kisicho na nguvu; na k**a warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe"
1 Pet 3:1‭-‬7

Mahubiri yenye nguvu ambayo wapagani na wasiookoka wanaweza kuyaelewa ni maisha ya mwenye haki.

Maisha yasiyo na kona, ya kumcha BWANA yanamuinua mtu.,hata kiuchumi.

Injili ya mtu yenye kuonekana kwenye maisha yake ndio injili ya nguvu inayoweza kubadilisha watenda dhambi.

6. Kuwa mshirika na mfuasi mwaminifu wa anayekuongoza.
Ebrania 13: 7 ,17, 24
"Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao. Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, k**a watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi. Wasalimuni wote wenye kuwaongoza, na watakatifu wote; hao walio wa Italia wanawasalimu."

Kuiga imani yao
ni kufanya vile wanafanya. K**a ni mtu wa kuheshimu ibada, heshimu ibada, ni watu wa kuheshimu ndoa na familia, heshimu ndoa yako na familia yako, kwenye malezi wako strict ,iga. Hadi uvaaji, iga. Iga Neno, maombi, bidii ya kazi , iga kila maisha mazuri wanayo yaonesha (Portraying) mbele yako.

Mungu anapokupa mchungaji wa kukuongoza, maana yake anakupa mfumo wa kufuata (pattern). Ndio maana inaweza kufika mahali washirika wakawa wanaomba k**a mchungaji, wanafundisha k**a mchungaji wao nk..

Watiini na kuwanyeyekea;
Ili kondoo wapate faida lazima mchungaji awe na furaha. Mchungaji akiwa hana furaha haitawafaidia washirika.

Wasalimuni wenye kuwaongoza;
Mungu amewaweka k**a vipaumbele, kila mtu anastahili salamu na heshima ila yule anayekuongoza awe wa kwanza.

Kumfuata mtu ni;
1. Kumfuata Mungu wake

2. Kufuata tabia zake njema, matendo yake mema yote.

3. Kumfuata mtu ni kumuiga mtu, anavyoheshimu watu wengine.
1Korintho 11:1
4. Kumfuata mtu ni kumfuata k**a anavyokuwa anamfuata Kristo.

5.Ufuasi ni kufanya kwanza halafu maswali baadaye.

Wajibu wa saba wa mshirika,
7. Ufuatiliaji wa washirika wapya.
Kila mgeni ambaye unamleta kanisani lazima umfatilie maana wewe ndio unamjua. Mfatilie anapoishi, upajue , uombe nae ili iwe rahisi kumfikia.
Hakikisha unajua hali yake ya maisha. Maisha yanatofautiana, kuna wenye maisha mazuri na wenye maisha magumu. Ukimfatilia ukijua ana maisha magumu na hatarishi kwa wokovu anaweza kurudi nyuma.

Kanisa ni familia ya Kiroho.
Lazima tujuane. Tusifurahie wakiokoka tu, ila tuwafuatilie kwa ukaribu.

Kuja nae ibadani walau mara 4 kwa mwezi.
Akija mwezi mzima, sio rahisi kurudi nyuma.

Kuwasilisha changamoto na matatizo yao kwa kiongozi. Mshirika ni daraja kati ya waongofu wapya, wageni na mchungaji au wazee, viongozi wa kanisa.

Kusimama kwao kwa niaba ya kanisa na mchungaji.
Kanisa likishakuwa la maelfu, mchungaji hawezi kuona kila mmoja mmoja, hapo Mshirika anakuwa mchungaji badala ya mchungaji, kiongozi wake kwa niaba ya kiongozi.

Kuna wageni wakija jambo la kwanza wanaloona ni mapungufu. Wakiona mapungufu badala ya kuwa-crush au kuungana nao, unawaelezea kwa upendo.
Usiwe mmoja wa wanaoliponda kanisa au mchungaji wako, uwe mtetezi na muokoa jahazi.

*****Mwisho*****
KARIBU KWENYE SEMINA YA SIKU 8 INAYOENDELEA HAPA KANISANI ABC KAHAMA,NYAHANGA KIVULINI.

FUATILIA IBADA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII
Facebook: Dickson Cornel Kabigumila
YouTube: Pastor Dickson Kabigumila

MAWASILIANO
Pastor Ibrahim Amasi
+255763706469
Askofu Dickson Cornel Kabigumila
+255 655 466 675

With Love, Karibu sana!
Alhamisi, 06-10-2023.

ABC GLOBAL KAHAMA MORNING GLORY SESSION DAY 55.10.2023WAJIBU WA MSHIRIKA KATIKA UKUAJI WA  MSHIRIKA
05/10/2023

ABC GLOBAL KAHAMA
MORNING GLORY SESSION DAY 5
5.10.2023

WAJIBU WA MSHIRIKA KATIKA UKUAJI WA MSHIRIKA




Address

Mbezi Beach Africana
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 21:00
Tuesday 08:00 - 21:00
Wednesday 08:00 - 21:00
Thursday 08:00 - 21:00
Friday 08:00 - 21:00
Saturday 08:00 - 21:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maju global products posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Maju global products:

Shortcuts

Share