05/12/2022
KOCHA CHARLES BONIFACE MKWASA AJIUZULU
Kocha Mkuu wa Klabu ya Ruvu Shooting, Charles Boniface Mkwasa amejiuzulu kuifundisha timu hiyo kutokana na mfululizo wa matokeo mabaya kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.
Akizungumza na Mtangazaji Maulid Kitenge wa EFM, Mkwasa amesema kuwa amefikia uamuzi huo ili kutoa nafasi kwa watu wengine waende wakaendeleze pale ambapo ameishia huku akiiacha timu hiyo kwenye nafasi ya 15 ya msimamo ambayo ni ya pili kutoka mwisho.
“Labda filosofi yangu imeshindwa kufanya kazi hivyo natoa fursa kwa mtu mwingine,” amesema Mkwasa.
Mkwasa na Ruvu Shooting wamecheza michezo 15 hadi sasa, ushindi mara tatu, sare mbili na wamepoteza michezo kumi ambayo ni mingi kulinganisha na timu yao ya msimu uliopita.
Mzunguko wa kwanza umeisha wakiwa katika nafasi mbaya, wakiwa wamepoteza mechi mechi nne mfululizo mpaka sasa huku mara yao ya mwisho kupata ushindi ilikuwa ni Septemba 29 na sasa ni Desemba.
Mechi inayofuata watamenyana dhidi ya Ihefu ambao nao wanajikongoja kujinasua kutoka chini kwenye msimamo wasije angukia play offs au kushuka daraja tena.
Hivyo timu hiyo sasa haina kocha.