17/04/2026
Namna ya Kununua Bidhaa na kufanya malipo Ndani ya KibubuApp
1. Kuchagua Bidhaa
Ukishafungua KibubuApp na kuchagua bidhaa unayotaka, chini ya maelezo ya bidhaa utaona chaguzi mbili:
• LIPA SASA
• LIPA KIDOGO KIDOGO
2. LIPA SASA
Ukichagua LIPA SASA, mfumo utakuelekeza kwenye hatua ya kujaza taarifa za anuani (address details) ili bidhaa iweze kuletwa mahali sahihi.
Baada ya kujaza anuani zako, utaelekezwa kwenye ukurasa wa malipo ambapo unaweza kuchagua njia ifuatayo:
• Wallet (Kibubu Wallet)
• Selcom
• AzamPay
Baada ya kuchagua njia ya malipo, utachagua tena kati ya:
• Card (Visa, Mastercard, n.k.)
• Mobile Wallet (mitandao ya simu)
Iwapo utachagua kulipa kupitia Kibubu Wallet, na k**a wallet ina salio la kutosha kulingana na bei ya bidhaa unayolipia, kiasi husika kitakatwa moja kwa moja na malipo yatakamilika.
3. LIPA KIDOGO KIDOGO
Iwapo utachagua LIPA KIDOGO KIDOGO, utaanza kwa kujaza taarifa zako za anuani kisha utaelekezwa kwenye malipo.
Kwenye hatua ya malipo, unatakiwa kuweka kiasi kisichopungua TZS 2,000 k**a malipo ya kwanza.
Mnunuzi anapewa muda wa hadi siku 90 kukamilisha malipo ya bidhaa anayolipia kidogo kidogo.
4. Jinsi ya Kuendelea Kulipia Bidhaa (Installments)
Ili kuendelea kulipia bidhaa uliyolipa kidogo kidogo, ingia kwenye akaunti yako na chagua:
• My Orders
Kwenye My Orders utaona orodha ya orders zako zote. Chagua order unayotaka kuendelea kulipia.
Utakapofungua order husika, utaona kitufe cha ‘LIPA KIDOGO KIDOGO’. Ukibofya hapo, utapelekwa moja kwa moja kwenye ukurasa wa malipo ili kuendelea kulipa.
Kila unapofanya malipo, kiasi ulicholipia tayari kitaoneshwa kwenye My Orders pamoja na muda uliosalia kukamilisha malipo ndani ya siku 90.
Karibu sana uendelee kupata huduma bora na yenye usalama 💯ukiwa na app ya