11/08/2025
Kila Mwamini Ana Imani.
Huwezi kwa namna yoyote kuzungumzia somo la Imani pasipo kuingia katika sura ya 11 ya Marko, kwa sababu katika kifungu hiki cha andiko ndiko kauli za kushangaza, na kusisimua, kauli nzuri ajabu juu ya somo la Imani zilipata kunenwa kutoka kinywani mwa Bwana.
MARKO 11:22-26
Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu.
Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.
Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.
Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Lakini k**a ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]
Nilichofanya katika kitabu hiki ni kuweka majumuisho ya vitu saba muhimu kuhusu somo la Imani. Na ukweli wa kwanza muhimu kuhusu Imani ni: kila mwamini ana kiasi fulani cha aina ya Imani-ya kiungu.
Nilizoea kufanya mikutano ya muda mrefu. Kwa miaka mingi sikukubali mwaliko wowote chini ya majuma matatu. Tungefanya mikutano kwa makanisa mitaani, na wakati mwingine tuliweka mikutano yetu wenyewe.
Katika siku hizo, nisingekubali mwaliko chini ya majuma matatu. Na mara nyingi tulikaa sehemu moja kwa majuma manne hadi nane. Wakati mmoja tulikaa majuma tisa. Tulifanya ibada mbili kwa siku, siku tano kwa wiki.
Ndiyo, tulipokaa muda mrefu hivyo β hasa majuma manne hadi tisa β tulikuwa na muda wa kutosha kuangalia kila kitu kinachohusu somo la Imani na kupindua kila jiwe na kukagua kila mwamba. Kwa mfano, tulizungumzia vitu k**a, Ikiwa Imani yako haifanyi kazi, ni kwanini haifanyi kazi? Tungelishughulikia hili na maeneo mengine ya Imani, na tuliita hiyo "Kliniki ya Imani."
Lakini unapokuwa katika mkutano na watu kwa muda wa wiki moja tu, na una ibada tano au sita tu, unalazimika kuminya somo lako na kuwapa kwa namna ya dozi. Kwa maneno mengine, unawapa tu yale yaliyo ya msingi katika somo la Imani, yaliyobaki unayaacha.
Hivyo katika kitabu hiki, nitakuongoza katika uelekeo sahihi. Halafu utaendelea mwenyewe kujifunza mengine juu ya imani.
Zingatia Marko 11:22 ya andiko letu: "Yesu akajibu akamwambia, Mwaminini Mungu." Maelezo ya tafsiri ya Bibllia ya Mfalme James yanasoma kwamba Yesu alisema, ". . . Iweni na imani ya Mungu."
Tafsiri nyingine inasoma (kwa kweli, Wasomi wa Kigiriki wanatuambia ndio tafsiri yake Orijino): "Iweni na imani ya Mungu." Kwa ufasaha kabisa, Yesu alisema, "Iweni na Imani ya Mungu!"
-Kenneth E. Hagin.