22/02/2026
Surah Al-Mu'minun
Surah Al-Mu'minun
بِسْمِ اللّٰهِ الرَّحْمٰنِ الرَّحِيْمِ
قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَ
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَنِ اللَّغْوِ مُعْرِضُونَ
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
وَالَّذِينَ هُمْ لِلزَّكَاةِ فَاعِلُونَ
Na ambao wanatoa Zaka,
وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ
Na ambao wanazilinda tupu zao,
إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَوَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
أُولَٰئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ
Hao ndio warithi,
الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن سُلَالَةٍ مِّن طِينٍ
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
ثُمَّ جَعَلْنَاهُ نُطْفَةً فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
ثُمَّ خَلَقْنَا النُّطْفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقْنَا الْعَلَقَةَ مُضْغَةً فَخَلَقْنَا الْمُضْغَةَ عِظَامًا فَكَسَوْنَا الْعِظَامَ لَحْمًا ثُمَّ أَنشَأْنَاهُ خَلْقًا آخَرَ ۚ فَتَبَارَكَ اللَّهُ أَحْسَنُ الْخَالِقِينَ
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.