OPSON GROUP

OPSON GROUP LUBRICANTS,
OIL FILTERS,
BRAKE PADS.,
BRAKE SHOE
CV JOITS,
U BOLTS,
FUEL PUMP,
BRAKE CHAMBER FOR
HOW,FAW,SCANIA

🌍 OPSON GROUP LIMITED
A diversified group of companies focused on Agriculture, Value Addition, Trade & Export. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

🌱 Kilimo cha Kisasa
🏭 Uongezaji Thamani wa Mazao ya Kilimo
πŸ“¦ Exportation ya Mazao na Bidhaa za Tanzania

24/05/2026

Kwanini kijana akimiliki kampuni anatengwa kwenye baadhi ya fursa zinazowahusu vijana?
Mfano kampuni ya kijana imetengwa kwenye special group pale Nest
Mfano mwingine kampuni ya kijana hairuhusiwi kupata mkopo wa 10% halmashauri lazima uwe kwenye kikundi.

Mmetumia vigezo gani kuwakataa vijana wanaomiliki kampuni?
Joel Nanauka
Waziri Wa Vijana
Ofisi ya Waziri Mkuu

Mpaka sasa hii ni ndoto. Ni mambo yanayoonekana kwa macho ya rohoni. Nikuhakikishie mdhamini wa hili ni Yesu Kristo mwen...
24/05/2026

Mpaka sasa hii ni ndoto. Ni mambo yanayoonekana kwa macho ya rohoni.
Nikuhakikishie mdhamini wa hili ni Yesu Kristo mwenyewe
Sijui itakua ila najua atafanya.
Sote tutaona kwa macho haya ya damu na nyama
Utukufu apewe Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo anaetupa zaidi ya tuombavyo au tuwazavyo.

19/05/2026

Mh waziri wa vijana Waziri Wa Vijana Joel Nanauka naomba utusaidie kampuni zinazomilikiwa na vijana ziweze kuingia kwenye special group kwenye mfumo wa NeST

KUJENGA MFUMO IMARA WA USAZAJI WA KARANGA TANZANIATanzania ina uwezo mkubwa katika uzalishaji wa karanga, lakini mfumo w...
19/05/2026

KUJENGA MFUMO IMARA WA USAZAJI WA KARANGA TANZANIA
Tanzania ina uwezo mkubwa katika uzalishaji wa karanga, lakini mfumo wa usambazaji bado haujapangwa vizuri na haujakidhi mahitaji ya wanunuzi wakubwa wa ndani na nje ya nchi.

Makampuni mengi ya usindikaji na export yanakutana na changamoto hizi:
Upatikanaji usio wa uhakika wa bidhaa
Ubora usiofanana
Kukosekana kwa mtandao rasmi wa wakulima
Hilo ndilo tatizo tunalolenga kulitatua.

TUNACHOJENGA
Kupitia OPSON GROUP LIMITED, tunajenga mtandao rasmi wa uzalishaji na usambazaji wa karanga tukianza na wakulima wadogo Tanzania.
Mfumo wetu unalenga:
β€’ Kuwaunganisha wakulima katika vikundi vya uzalishaji vilivyoratibiwa
β€’ Kuwapa mafunzo ya kilimo bora cha karanga
β€’ Kuhakikisha uvunaji, uchambuzi, na uhifadhi wenye viwango vya ubora
β€’ Kujenga mfumo wa usambazaji wa uhakika kwa wanunuzi wa viwandani na export market

MAONO YETU
Tunajenga daraja la kuaminika kati ya wakulima na wanunuzi wa karanga kwa kuhakikisha:
β€’ Upatikanaji endelevu wa karanga bora
β€’ Uzalishaji wenye uwezo wa kukua
β€’ Mfumo wa ufuatiliaji wa bidhaa kutoka shambani hadi sokoni
β€’ Mikataba ya muda mrefu ya usambazaji

USHIRIKIANO WAZI
Kwa sasa tupo wazi kushirikiana na makampuni ya usindikaji, exporters, wawekezaji, na wadau wa kilimo wanaohitaji bidhaa za uhakika.
Katika hatua hii ya mwanzo, tunatafuta ushirikiano kwenye maeneo yafuatayo:
β€’ Mafunzo kwa wakulima
β€’ Vifaa vya uzalishaji na uhifadhi
β€’ Ushauri wa viwango vya ubora
β€’ Ujenzi wa mfumo rasmi wa usambazaji
Kwa kushirikiana nasi mapema, wadau watapata nafasi ya kwanza katika mtandao unaokua wa biashara ya karanga Tanzania.

LENGO LETU
Kujenga mfumo endelevu wa biashara ya karanga Tanzania unaowanufaisha:
β€’ Wakulima wadogo kupitia kipato na soko la uhakika
β€’ Wanunuzi na viwanda kupitia upatikanaji wa bidhaa bora na za kutosha
Tunakaribisha ushirikiano kutoka kwa makampuni ya usindikaji, wawekezaji, na wadau wa agribusiness wanaotaka kushiriki kujenga mfumo rasmi wa biashara ya karanga Tanzania.
Kwa sasa tunaanza na pilot phase huku tukiwa wazi kupokea ushauri wa kitaalamu na kimkakati kutoka kwa wadau wa sekta hii.

Nahitaji ule mkona uliobeba budget ya wizara ya afya 2026/27 niweze kuaza safari ya kuelekea hii ndoto
17/05/2026

Nahitaji ule mkona uliobeba budget ya wizara ya afya 2026/27 niweze kuaza safari ya kuelekea hii ndoto

Niseme ukweli k**a itanihitaji Figo ili niweze kupata hela ya kuanza safari ya kuifikia hii ndoto yangu niko tayari.
14/05/2026

Niseme ukweli k**a itanihitaji Figo ili niweze kupata hela ya kuanza safari ya kuifikia hii ndoto yangu niko tayari.

Hawa ni viongozi wa makampuni makubwa ya marekani walioko kwenye msafara wa Rais wa Marekani nchini China. Umegundua nin...
13/05/2026

Hawa ni viongozi wa makampuni makubwa ya marekani walioko kwenye msafara wa Rais wa Marekani nchini China. Umegundua nini?

13/05/2026

SIOGOPI CHOCHOTE. YAANI SINA CHA KUOGOPA

Iko hivi ikitokea nahitaji kulipa gharama kadhaa ili kufikia ndoto zangu niko tayari kuzilipia. K**a itahitajika aibu, kudharauliwa, nguvu zangu niko tayari kuzilipia

UWEKEZAJI WA KILIMO WENYE FAIDA KUBWA AMBAO WAWEKEZAJI WENYE AKILI WANAULENGAKilimo bado ni moja ya njia za haraka zaidi...
12/05/2026

UWEKEZAJI WA KILIMO WENYE FAIDA KUBWA AMBAO WAWEKEZAJI WENYE AKILI WANAULENGA

Kilimo bado ni moja ya njia za haraka zaidi za kutengeneza utajiri, lakini wawekezaji wenye akili huwekeza kwenye maeneo yenye mzunguko wa haraka wa fedha na mahitaji ya uhakika sokoni. Uwekezaji wenye faida kubwa leo ni ule unaochanganya kasi, uwezo wa kukua, na kuongeza thamani.

Ufugaji wa kuku ni biashara inayorudisha mtaji kwa haraka. Ndani ya wiki 6 hadi 8, kuku wa nyama huwa tayari kuuzwa, huku uzalishaji wa mayai ukitoa mapato ya kila siku. Ufugaji wa samaki pia ni mgodi wa dhahabu, hasa uzalishaji wa kambale, unaochochewa na mahitaji makubwa ya protini na ukuaji wa masoko ya mijini.

Kilimo cha mboga kwenye greenhouse kina faida kubwa sana kwa sababu mazao k**a nyanya, matango, pilipili, na lettuce hukomaa haraka na huuzwa kwa bei nzuri mwaka mzima. Usindikaji wa muhogo, mashine za kusaga mpunga, na uzalishaji wa mafuta ya mawese pia vinaendelea kuwa na faida kubwa kutokana na matumizi makubwa ya ndani na mahitaji ya viwandani.

Usindikaji wa mazao ya kilimo ndipo pesa halisi huzidishwa. Wawekezaji wanaochakata mazao mabichi kuwa bidhaa zilizofungashwa hupata zaidi kuliko wanaouza mazao ghafi. Maghala ya kuhifadhi, mifumo ya cold-chain logistics, uzalishaji wa chakula cha mifugo, na huduma za kilimo cha kisasa kwa mashine pia vinaibuka k**a fursa kubwa za uwekezaji.

Mustakabali ni wa wawekezaji wanaoona kilimo si k**a kujikimu tu, bali k**a mfumo wa kisasa wa biashara unaotumia teknolojia, mitambo, ubunifu, na taarifa za soko.

Sisi k**a kampuni ya OPSON GROUP LIMITED tumelenga kuchakata na kuongeza thamani mazao ya kilimo na kulisha Tanzania, Afrika Mashariki na dunia kwa ujumla. Kwasasa tunahitaji mtaji wa kuanza usiozidi millions 50 huu tutautumia kununua na kuuza mazao k**a maharage na mahindi na kuuza nchi jirani k**a Kenya lakini tutafanya biashara ya kununua unga kutoka NFRA na kusambaza kwa kutumia channels mbalimbali, Faida tutakayoipata kwenye biashara hizi za mwanzo tutazitumia kufanya kilimo na kujenga viwanda vya kuongeza thamani mazao k**a mahindi, karanga,na Alzeti kwa kushirikiana na serikali na sector nyingine binafsi k**a banks ikiwepo bank ya kilimo

Sisi tunaamini katika uchumi wa leo, kilimo si suala la kulisha watu tu β€” ni kujenga utajiri, kuunda ajira, na kudhibiti mustakabali.

12/05/2026

Ukimsikiliza Rostam Aziz, anakufundisha kwamba dunia ya sasa si dunia ya kusubiri kusaidiwa. Si dunia ya kulalamika na kusema β€œna sisi tunataka haki yetu.” Ni dunia ya kupambana, kujituma, kutumia akili, na kujitengenezea njia mpaka upate haki yako.
Leo anayesonga mbele si yule anayesubiri huruma, bali ni yule anayechukua hatua.

Fursa zipo kwa wanaothubutu, wanaofanya kazi kwa bidii, na wanaokataa kukata tamaa. Dunia ya leo inamheshimu mpambanaji.

Ndoto zote kubwa huanza k**a mbegu ndogo sana ardhini.Hiyo mbegu ndogo ina maana kubwa kuliko chochote. Maisha yanaweza ...
12/05/2026

Ndoto zote kubwa huanza k**a mbegu ndogo sana ardhini.

Hiyo mbegu ndogo ina maana kubwa kuliko chochote. Maisha yanaweza kutuvuruga, lakini tutapambana kurekebisha mambo na kusimama tena. Tunakuwa bora kimya kimya, mbali na macho ya watu.

Na hatua kwa hatua tutajaribu kubadilisha maisha ya kila mmoja.
Haijalishi itachukua muda gani, au itaonekana polepole kiasi gani, lakini tutafanikiwa.

Address

Dar Es Salaam
1210

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

+255786575735

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when OPSON GROUP posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to OPSON GROUP:

Share