OPSON GROUP

OPSON GROUP LUBRICANTS,
OIL FILTERS,
BRAKE PADS.,
BRAKE SHOE
CV JOITS,
U BOLTS,
FUEL PUMP,
BRAKE CHAMBER FOR
HOW,FAW,SCANIA

๐ŸŒ OPSON GROUP LIMITED
A diversified group of companies focused on Agriculture, Value Addition, Trade & Export. ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

๐ŸŒฑ Kilimo cha Kisasa
๐Ÿญ Uongezaji Thamani wa Mazao ya Kilimo
๐Ÿ“ฆ Exportation ya Mazao na Bidhaa za Tanzania

Unajua nini kuhusu dira ya 2050? Unajua mtoto atakaezaliwa leo atakua na miaka 24?Unajua tunaweza tukawa na idadi zaidi ...
14/08/2026

Unajua nini kuhusu dira ya 2050?
Unajua mtoto atakaezaliwa leo atakua na miaka 24?
Unajua tunaweza tukawa na idadi zaidi ya watu millions 120?
Unajua pato la taifa linatakiwa kuwa trillion 1 kwa mwaka? Leo ni billion 90 kwa mwaka.
Inabidi uchumi ukue kwa zaidi ya 11%.
Sector binafsi imebebeshwa jukumu hili kwa 70%
Vijana wanahitajka kuchangia kwenye safari hii kwa 70%

Tunahitaji sector ya kilimo ichangie Dira hii kwa zaidi ya 40% hii inawesekana kwa mwaka kilimo kikatupa zaidi ya billions 400. Nasema hivi kwasababu nchini ndogo k**a Uholanzi yenye ukubwa sawa na dodoma inaingiza billions 200 kwa mwaka mapato ya kilimo tu peke yake.

Tukiwa serious na kilimo pekee kinaweza kutufukisha kwenye lengo la pato la usd trilioni moja kwa mwaka hata kabla ya 2050.

Nataka kusema nini? Ni hivi pato la usd trilioni 1 kwa mwaka kwa nchi k**a Tanzania inawezakana ikiwa tutaamua kuwa serious na kuacha maneno na kufanya vitendo.

Lazima serikali ichukue hatua za makusudi kuhakikisha kundi kubwa la sector binafsi na vijana wanafanya kazi kwa kuwezeshwa kufanya kazi. Vijana wengi wana idea na uwezo wa kufanya kazi lakini wengi hawana mitaji na wanapishana na fursa k**a za kilimo. Nashangazwa na billions 200 za vijana alizotoa Rais mpaka sasa miezi 9 ziko bank zilitakiwa ziwe kazini zinazalisha. Punguzeni itafaki punguzeni vigezo lakini pia punguzeni matamasha wapeni vijana mitaji wafanyekazi nchi ianze hatua kuelekea 2050.

NANENANE
08/08/2026

NANENANE

15/07/2026

Uholanzi ina ukubwa sawa na mkoa wa Dodoma. Inaingia Tanzania mara 23. Siyo hivyo tu uholanza ina watu millions 19 ni moja ya nchi yenye msongamano wa watu sana. Siyo hivyo tuu waliwahi isogeza bahari wapate ardhi. Sio hivyo tuu watu wanaojihusisha na kilimo ni takribani laki 2. Hawajaishia hapo mapato yao yanaotokana na kilimo ni takribani billions 200$. Tanzania tuna watu millions 20 wanaojihusisha na kilimo na mapato yetu ni billions 3.8$. Pale Uholanzi mwaka 2025 uzalishaji wa nyama, mayai na maziwa yaliingiza billions 23$ sawa nq budget ya Tanzania 2026/27.

Sasa sisi Tanzania si tuna dira ya 2050 yenye lengo ya kufika pato la trilions 1$ kwa mwaka? Ili tufike huku lazima tujifunze kutoka uholanzi kwenye sector ya kilimo. Tukajifunze uzalishaji na ujasiriamali kutoka China.
Joel Nanauka
Waziri Wa Vijana
Ikulu Mawasiliano
Aje-Farms Mashamba Yanayotembea

Mh Joel Nanauka hii ni invoice nilipokea kutoka kwa kampuni wanayonifanyia uhasibu kwenye kampuni yangu ya OPSON GROUP L...
15/07/2026

Mh Joel Nanauka hii ni invoice nilipokea kutoka kwa kampuni wanayonifanyia uhasibu kwenye kampuni yangu ya OPSON GROUP LIMITED. Mheshimiwa waziri nilifarijika sana baada ya Mheshimiwa Rais kutoa ahadi na kuitekeleza kwa kutoa bilions 200 kwa ajili ya kusaidia kampuni changa za vijana.

Mheshimiwa waziri kampuni yangu ina leseni ya kufanya usafi na nimejsajili Nest lakini k**a kampuni changa natakiwa kushindana na kampuni kubwa za usafi k**a SUMA JKT unakuta Masharti ya kupata tenda husika lazima niwe nilishafanya kazi za millions 50 tangu 2023 na kampuni nimeisajili mwaka jana na leseni nimepata mwaka huu hivyo automatically kampuni inakosa vigezo na kukosa fursa ya kufanya kazi ninayoweza kuifanya.

Lakini kupitia special group haya masharti hayapo na k**a yapo yanakuwaga nafuu sana. Inasikitisha sana kampuni za vijana kukosa fursa hii sababu ni kampuni na sio kikundi. Mheshimiwa waziri kwa maoni yangu hii sio sawa na lipo ndani ya uwezo wako kurekebisha sheria hii ili iendeane na nia ya Mheshimiwa Rais Samia kuwezesha kampuni changa za vijana. Kampuni za vijana ziweze kupata tenda k**a special group kwanini kijana kusajili kampuni iwe kosa na kumtoa kwenye baadhi ya fursa za vijana? Ili hali ni kijana alieamua kurasimisha biashara zake na kulipa kodi halali hata kabla ya kuanza kazi?

Mheshimiwa waziri nimekuandikia hili k**a kijana kutoka wilaya ya ilala niliejaribu kufatilia fursa zote zilizotolewa na wizara ya vijana na bahati mbaya sana sijabahatika kupata fursa hizo. Mheshimiwa waziri wilaya ya ilala ina hospital mpya na mradi wa mwendokasi utakaonza mwaka huu nilitamani sana kuona kampuni za vijana wa Ilala zikipata fursa za kutoa huduma ya usafi kwenye miradi hii.

โ€œKwahiyo maziwa ya mtoto wangu ndo unamchemshia mtoto wako?โ€
10/07/2026

โ€œKwahiyo maziwa ya mtoto wangu ndo unamchemshia mtoto wako?โ€

08/07/2026
07/07/2026

Ishi na watu vizuri

07/07/2026

KWA BIASHARA HII UNAWEZA KUTENGENEZA MILLIONS 6 KWA MWEZI

Nimetumia siku 45 kujifunza biashara ya tairi za magari. Nilichojifunza ni miongoni mwa biashara nzuri sana kumbuka hii ni biashara ilioko kwenye mnyororo wa biashara ya usafirisaji k**a unavyojua biashara ya usafirishaji ni moja ya biashara kubwa sana.

Kwa siku 45 nimejua machimbo yote yaani supplier wa tairi kubwa na ndogo kwa jiji la Dar es salaam. Hii tairi ukiiuchukia kwa bei ya jumla na kuuza kwa wateja wa rejareja kila tairi una faida ya tsh 20,000. Zipo mbinu mbalimbali za kuuza nimejifunza kwenye hii biashara kwa muda wa hizi siku 45.

Nilizijaribu njia hizi kwa muda wa siku 14 kila wiki niliweza kuuza tairi 20. Tulikubaliana na mwenye mzigo nataka kujifunza hivyo aliweza kunifundisha njia zote ma machimbo yote lakini kila tairi niliokua nauza alikua ananipa elfu 5 k**a commission.

Sasa sikia hiyo biashara ukiamua kuifanya kwa njia nzuri kwa mwezi unaweza kuuza tairi 100 huu ni uhakika kabisa. Biashara ikizoeleka kwa mwezi unaweza kuuza mpaka tairi 300. Sasa piga tairi 300 mara faida ya elf 20. Hapo una millions 6 k**a faida.

Hapo unahitaji mtaji wa millions 15 tu kuanza kutengeneza millions 6 kila mwezi.

Usione hii biashara wanafanya wahindi na waarabu ukaichukulia poa aisee.

Hata sasa ukitaka tairi kubwa na ndogo nicheki
MIXER =440,000
HIGHWAY =440,000
DIFF=480,000
SUPERSINGLE FUPI =680,000
SUPERSINGLE NDEFU =580,000

USAFIRI KWA DAR NI BURE

OPSON GROUP LIMITED โ€“ PROFESSIONAL CLEANING SERVICES Je, unahitaji mazingira safi na yenye kuvutia kwa biashara au makaz...
25/06/2026

OPSON GROUP LIMITED โ€“ PROFESSIONAL CLEANING SERVICES
Je, unahitaji mazingira safi na yenye kuvutia kwa biashara au makazi yako?

Tunatoa huduma za usafi wa kiwango cha juu kwa:
Ofisi
Nyumba za Makazi
Shule na Vyuo
Hoteli na Guest Houses
Hospitali na Kliniki
Maduka na Majengo ya Biashara
Apartments na Residential Compounds

Huduma zetu ni pamoja na:
โœ… Daily Cleaning
โœ… Deep Cleaning
โœ… Post-Construction Cleaning
โœ… Office Cleaning
โœ… Residential Cleaning
โœ… Supply of Professional Cleaners

Kwa nini utuchague?
โœ”๏ธ Wafanyakazi waaminifu na wenye mafunzo โœ”๏ธ Huduma za uhakika na za wakati โœ”๏ธ Bei nafuu na zinazoshindana sokoni โœ”๏ธ Ubora unaoridhisha

๐ŸŒŸ Tunasafisha kwa umakini ili wewe ujikite kwenye kazi zako muhimu.
๐Ÿ“ž Wasiliana nasi leo kwa maelezo zaidi na kupata quotation ya bure.
0786575735,0753929166

OPSON GROUP LIMITED Your Trusted Cleaning Partner.

23/06/2026

Mtafute Mungu, mtumikie Mungu, Mungu akutawale.
Tafuta fedha,
Miliki fedha, itawale fedha na hakikisha inakutumikia.

Address

Dar Es Salaam
1210

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

+255786575735

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when OPSON GROUP posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to OPSON GROUP:

Shortcuts

Share