26/12/2019
Kwa ukweli kuwa katika maeneo matukufu hasa karibu na nyumba tukufu Al_Kaaba ni habari nyingine ambayo haielezeki kwa maneno.
Ni hisia za ndani ya moyo za furaha zizoelezeka kwa maneno na kalamu. Allah Atuwafikishe kila mmoja wete aweze kupata furaha na raha hii ya kuwepo maeneo haya matakatifu, kuswali Swala za faradhi na sunna, kuiangalia Al Kaaba, Makamu Ibrahim, Kunywa maji ya zamzam, kuvaa Ihram, kutufu, kufanya sai, na kunyoa Nywele. Kutembelea maeneo matakatifu, Masjid Raya, Masjid Jinn, Masjid Shajara, Alipozikwa mama yetu Bi Khadija _ mke wa Mtume. Kuzuri nyumba aliyozaliwa Bwana Mtume. Kuona sehemu ilipokuwepo nyumba ya Bi Khadija. Sehemu ilipokuwepo nyumba ya Sayyidna Abubakar na Sayyidna Umar Allah Awawie radhi.
Raha na furaha isiyo kifani unapofika Madina na kuswali ndani ya Msikiti wa Bwana Mtume. Kuzuru kaburi lake na makaburi ya marafiki zake na masahaba wake vipenzi Sayyidna Abubakar na Sayyidna Umar Allah Awawie Radhi. kuzuru Baqii _ sehemu waliyolala masahaba zaidi ya elfu tatu Na kuzuru Masjid Ali Allah Amuwie radhi, Masjid Ghamama, Masjid Abubakar, Saqifa Banu Saida, Masjid Abudhar, Masjid Quba, Masjid Qiblatein, Mlima Uhud n.k
Alhamdulillah kuzuru maeneo haya ya kihistoria kunatupa furaha isiyo na maelezo.
Kwa ukweli nashindwa kueleza furaha na hisia njema nilizozipata katika kuzuru maeneo haya yenye historia kubwa ya Uislamu.
Allah Atuwafikishe kwa neema hii ya Uislamu tuwe waja wake wema hapa duniani.
Waja ambao watawasaidia wanaadamu wenzao katika kuwajenga kiroho, kiakili, kihisia, kijamii na kiuchumi.
Waja ambao wanajisalimisha kwa Muumba wao.
Waja ambao wanaheshimu utu na ubinaadamu wa wenzao kwa kuenzi na kulinda uhai wao, mali zao na heshima zao.
Waja ambao wanakuwa ni chemchemu ya mambo ya kheri kwa ajili ya maendeleo yao binafsi, familia zao, taasisi zao, na nchi yao. Amin