22/01/2025
“Basi tabiri, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli. Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu. Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, BWANA, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema BWANA.” Eze 37:12-14
BWANA ATUTENDEE HAYA:-
1. Afunue makaburi yetu.
2. Atupandishe kutoka katika makaburi yetu,
3. Tuwe watu wake.
4. Atie roho yake ndani yetu.
5. Atufanye tuishi,
6. Atuweke katika nchi yetu, Destiny yetu.
Nasi tutajua ya kuwa , BWANA, amesema na kuyatenda hayo.
Katika Jina la Yesu.