ELIMU YA NDOA

ELIMU YA NDOA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ELIMU YA NDOA, Shopping & retail, Azizi ally uwanja wa sifa, Dar es Salaam.

WAJIBU WAKUTENGEZA NDOA IMARA LIPO MIKONONI MWAKO KWANZA TAMBUA NDOA UJENGWA KWA UPENDO,HESHIMA,UAMINIFU NA USAWA.KAMA UNABIASHARA YAKO UNATAKA KUTANGAZA NIONE INBOX KWA MAELEWANO ZAIDIοΏ½οΏ½οΏ½οΏ½

01/07/2025

Mwenza wako amejua k**a umemchiti, baada ya kumuomba msamahaa unatarajia mambo yatakuwa k**a zamani mmmh ndugu yangu kuanzia hapo ndio mambo aya kadhaa yatazaliwa: 1) kutokuaminiana 2)kuzalauliana 3)kujibizana kila Mara 4) ata k**a utaenda msibani kuzika mwenzio atakuhisi umetoka kuonana Na mchepuko 5)mtaanza kupuuziana 6) usiri kati yenu 7)upendo kupungua namengine mengi. Nb: ukishaingia katika mahusiano fanya makosa yote utasamehewa ila epuka kumsaliti mwenza wako. Usaliti ndio kitu pekee kikubwa kinaumiza hisia kwa haraka kuliko hata kidonda. ASANTE.

04/09/2024

ZA MASIKU TELE FANS😍😍😍

01/03/2023

Taraka uwa inaandikwa vipi? Au ukiandika kwaaina gani itaonesha hii ni taraka aijalishi ni ya kikristo au kiislamπŸ™

MWENYE PESA ULA VITAMU Mwenye kuni ula vilivyo iva.
24/02/2023

MWENYE PESA ULA VITAMU

Mwenye kuni ula vilivyo iva.

24/02/2023

MUDA"
Habari member za siku nyingi na karibuni tena tuwe pamoja natumai mu wazima na tumekutana tena kwa wale waliotangulia mbele za mungu basi dua zetu mungu awapunguzie adhabu ya kaburi.

Leo nimeona nizungumze na ninyi kuhusu MUDA" hakikisha unatumia muda wako vizuri katika kila jambo unalolifanya wote tunajua kuwa wakati aumsubili mtu ivyo ni vyema nasi kufanya vitu kulingana na muda Leo muda tutautumia katika mahusiano k**a page yetu inavyotuambia.

Kwanini basi... Watu mmekuwa mkiumizana sana kwenye mahusiano yetu mnanyimana amani, watu wanaishi kwenye hayo mahusiano ni kwasababu tu, watu mpo kwenye ndoa ambazo aziwapi furaha ivi unajua kuishi sehemu ambayo haikupi amani na furaha ni kupoteza muda? Jibu ni ndio UNAPOTEZA WAKATI'

Ivyo basi hakikisha unampa furaha uliyenaye kwasababu wakati wa kufurahi ni mdogo sana kwenye hii dunia ambayo imegubikwa na wimbi la machozi na maumivu kutoka kwa watu tunaowapenda ebu jiulize unaishi kwa uzuni na mateso ukiwa duniani upati furaha kiasi kwamba unamsahau mungu umeacha mpaka kufanya ibada kwaajiri ya hayo majonzi uliyonayo na mwisho umauti unakujia then inasemekana pia ukishindwa kufanya mema duniani mbinguni ni moto swali linakuja hapa duniani umelia weeeeee ujapata furaha alafu mbinguni ww ni wa motoni sasa basi furaha yako wewe iko wapi?

Acheni kufanya vitu vinavyowakosesha amani watu wengine ishi maisha unayowish kuishi chagua furaha kwenye maisha yako lazimika kukaa mbali na vile vitu ambavyo ni chanzo cha uzuni yako, una haki ya kufurahi na kuishi maisha uyapendayo hata k**a auna kitu uyo isiwe sababu ya kutokuwa na furaha maisha ni mafupi sana. Usimbebe mtu moyoni mwako achilia hayo yanayokunyima amani wasamehee wote waliokukwaza anza upya tafuta furaha yako acha kulia kulia kutafuta huruma ya walimwengu mtafute mungu kwa bidii badilika kuwa mtu safi kuanzia Leo ili usife kwa majuto.πŸ’“πŸ’“πŸ’“πŸ’“πŸ’“πŸ’“πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™

10/11/2022

Kaka naomba msaada naishi nyumba ya kupanga na wapangaji wenzangu watatu mm nikiwa wa nne sasa mpangaji mwenzang mmoja ameolewa na mm nimetokea kumpenda uyo mwanaume yaani mapenzi kutoka moyoni nampenda sana uyu kaka shida inakuja mkewe ni mtu tulioshibana sana tunasaidiana kwa mambo mengi tatizo akija tu mumewe nakosa kujiamini najiskia aibu kumtazama lakini yeye ananitazama bila shida na aonyeshi k**a amevutiwa na Mimi na hali hii imepelekea mm kuwakataa mwanaume wengine kwaajiri yake naogopa asije niona na mwanaume napenda anione nipo single nisaidie nifanyeje nampenda sana sijui ni lini nimeanza kumpenda ila najikuta nampenda sana na ikitokea nikimuona wanacheka na mkewe nahisi wivu sana mpk nimeanza kumchukia mkewe.

ELIMU YA NDOA, pole dada kupenda sio dhambi ila tayar uyo ni mume wa mtu ni vibaya sana kuvunja ndoa ya mtu k**a uwezi kujizuia ni bora ukahama iyo nyumba au lah! Tafuta mwanaume ambaye anakupenda na uwe bize na uyo mchumba kuliko kumfikilia mwanaume wa mwenzio. Ukiziendekeza hisia zitakupeleka kombo tulia tafuta mume sahihi kwa ajiri yako na watoto wako wajao. Jukumu la kuwachagulia baba bora watoto wako lipo mikononi mwako.ASANTE

UNAWEZA UKAONGEZA USHAURI KWA MWENZETU.

09/11/2022

Ni mambo gani ambayo mume au mke akikufanyia kwenye ndoa yako yatakupa furaha na amani ya moyo na pia itakuwa ngumu kwa ww kufikilia kumsaliti ata kwa bahati mbayaπŸ€”

WENGINE TUNATAMANI KUTOKA KWENYE NDOA WENGINE WANATAMANI KUINGIA Hii ni kauli ambayo kwa sasa iko trending sana midomoni...
31/10/2022

WENGINE TUNATAMANI KUTOKA KWENYE NDOA WENGINE WANATAMANI KUINGIA
Hii ni kauli ambayo kwa sasa iko trending sana midomoni mwa baadhi ya wanandoa. Jamani ndoa zina raha sana k**a amjui ndoa ni tamu mno lakini k**a umeingia katika ndoa na mtu asiye sahihi basi kamwe uwezi ona utamu wa ndoa na yafuatayo ni mambo machache yatakayo kufanya ujue kwanini ndoa yako aina furaha ya kudumu.

1)kuoana na mtu ambae ameamua kuingia kwenye mahusiano baada tu ya umri kumtupa mkono pasipo kupata ndoa. Ukikutana na mtu uyu lazima mahusiano yasiwe na furaha kwasababu utakuwa umeingia kwenye ndoa na mtu ambae alichoka kuwa single ivyo aliitaji mtu ili nayeye umri usipite bila kuonja ndoa.

2)kukimbilia kuoa/kuolewa kwasababu Fulani kaowa/kuolewa mtu uyu pia awezi kukupa furaha kwasababu tamaa ndio iliyompeleka katika ndoa na sio utayari wake wa kuitaji kuowa/kuolewa

3)mtu ambae anampenda mtu mwingine. Watu saizi awapendani kwanza wanaingia katika ndoa ili mradi tu nae yupo ndoani, anampenda juma anaolewa na bakari na mwisho wa siku unajikuta ndoa aina amani

4)Siri(makando kando) hizi siri jamani Mara nyingi zinawapotezea uaminifu katika ndoa zenu na ndoa ambayo inasiri siri sana Mara nyingi aikosi migogoro kwasababu inaaminika kuwa mume na mke ni mwili mmoja sasa siri baina yenu zinatoka wapi?

5) kuzoeana ukishakuwa kwenye mahusiano ambayo mmezoeana sana mapenzi yenu upungua radha yanakuwa ayana mbwembwe tena jitaidini kila siku kuwa wapya na acheni na hile hali ya kujifanya umezoeana sana na mwenza wako. Madhara yakuzoeana ni pale mwenzio anaweza kukuambia jambo la msingi ila wewe automzingatia kisa tu umemzoea unamjua. Mapenzi ayana kuzoeana.

6)kulazimishwa kuoa/kuolewa kamwe usiingie kwenye ndoa kwa shinikizo la wazazi au ndugu kwasababu ndoa iyo aiwezi kukupa furaha. Tafuta mume au mke pindi uwapo tayari ukiwa na umri uliokomaa na ukiwa unafahamu ndoa ni nini.

7)kuoana na mwenza wako mkiwa bado nyote mnaumri mdogo au kuowana na mwenza mkiwa na umri sawasawa. Hapa amtakuwa na mawazo ya maisha zaidi ya s*x tu. Na usaliti kwenu itakuwa k**a unavokula ugari tu.kifupi mtapitia changamoto nyingi mno mpanga ndoa itakuwa chungu kwenu akuna wakumuongoza mwenzie.

Hakikisha unaolewa/kuoa mtu unaempenda ili ufurahie ndoa yako mpende akupende ili mnogeshe mahaba yenu fanyeni mambo kwa pamoja pendaneni,heshimiane mapenzi ni k**a mboga ili inoge inahitaji chumvi vivyo ivyo katika mapenzi kunaitaji vionjo ili penzi likoleee

MAZOEA:Leo nimeona niwakumbushe ndugu zangu kuna jambo uwa tunakosea na kuwakosea watu wengine kwenye maisha yao ya ndoa...
31/10/2022

MAZOEA:

Leo nimeona niwakumbushe ndugu zangu kuna jambo uwa tunakosea na kuwakosea watu wengine kwenye maisha yao ya ndoa.
Jamani ukishaona rafiki ilienae ameshakuwa mume au mke wa mtu basi jitaidini sana kupunguza mazoea yakijinga. Ndoa zinauma sana watu awana furaha na ndoa zao sababu ni sisi tumeziganda ndoa za watu. Mdada umeweka mazoea yaliyopitiliza na mume wa mtu ukimuona tu baba Fulani nisaidie hata elfu mbili hapo baba Fulani nisaidie vocha yaani aujali k**a uyo mume unaemuomba omba visent tayari ni mume wa mtu anatakiwa awe bize kulea familia yake ukimuona kujichekesha chekesha akuishi utazani umetekenywa tena ata ukimuona mkewe aujistukii wewe ni kujichekesha kwa mume wa mwenzio matarajio yako ni nini hasa utongozwe ili utembee nae ama?

Nawewe mwanaume ushajua mwenzio mke wa mtu bado auachi kumtumia meseji za ajabu ajabu Dada wa watu bila kujali unaweza kuharibu ndoa ya watu kwani mkisalimiana na kisha kila mmojawapo akaendelea na mambo yake aiwezekani acha kujifanya unamjali sana mke wa mwenzio wanawake ni wengi wanahitaji waume wakuwaoa usivunje ndoa ya mtu.

Kifupi tujifunze kuheshimu ndoa za watu tupunguze mazoea yasiyo na tija mambo yasiyona manufaa tusiyalete katika ndoa zawatu.

Can imagine jamaa anamnunulia mke wa mtu zawadi tena zawadi yenyewe utashangaa ni nguo ivi uko serious kweli umnunulie mke wa mwenzio nguo? Vipi mwenye mke akijua unadhani atahisi vipi?

Wanawake acheni kuwatumia tumia meseji waume za watu waacheni walee na kuwatunza watoto wao ata k**a ni rafiki tu kwako mtu akishakuwa mume au mke wa mtu kuna vitu baadhi upungua.

IVI TUMEELEWANA AU NDIO NAONGEA PEKEANGU HAPA?

πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”

WIVU WIVU kwanini unakubali wivu ukutese, wivu unakuharibia fraha ndani ya ndoa yako wivu unakupa stress, kibaya zaidi w...
18/10/2022

WIVU WIVU
kwanini unakubali wivu ukutese, wivu unakuharibia fraha ndani ya ndoa yako wivu unakupa stress, kibaya zaidi wivu ambao unakutesa wew ni wakujitafutia wewe mwenyew unajiumiza mwenyew kwa vipi basi k**a ww ni miongoni mwa watu wanaofanya hivi basi nakuapia mahusiano yako yamejaa stressπŸ€”πŸ€”πŸ€”.
1)k**a mwenzio akipigiwa simu unaacha kila unachofanya unatega sikio kusikilizia sauti inayotoka ndani ya simu uku ukiambatanisha hisia zako kumsoma na mpokeaji namna anavojibu NAKUAPIA UMEUMIA

2)k**a unavizia amelala au kaenda kuoga uibe simu yake ukague meseji na missed call NDUGU UTATESEKA SANA

3)k**a akiwa amezoeana na mwanamke au mwanaume mmoja wewe ukajua afu unaanza kujiuliza kwann awa wanamazoea kiasi iki itakuwa mtu wake HIZO HISIA ZITAKUUMIZA

4)k**a ukiwa unamchunguza kwenye simu yake na kila ukipekuwa unakuta no meseji no missed call no received call wala no dialing call na ukaanza kujiwazia kwann akuna hizo mambo uyu anamichepuko kafuta DEAR NIKUPE POLE

5)akichelewa kurudi au hata akiwahi kurudi unakimbilia kumnusa nguo labda utaskia marashi ya tofauti MY WANG UNAFELI

6)unaiba namba kwenye simu ya mwenzio afu unaanza kumpigia mmoja baada ya mmoja kuuliza anamahusiano gani na mtu wako UNAJIFERISHA

hivi utaishi kwa kujitesa mwenyew mpk lini kwanin unaupa moyo wako heka heka ulali vizuri unywi vizuri ucheki vizuri muda wote moyo unakuuma aufurahii ndoa yako?

Nikupe mbinu za kukufanya ili usiumie tena nataka ufurahie ndoa yako nakuonea huruma unautesa moyo.
1)k**a ulikuwa unamfatilia muache kuwa bize na mambo unayoyapenda sikiliza music mikali angalia muvi zako pendwa

2) kuwa bize kutafuta pesa hii itakufanya ukose muda wakuwaza ya mwenzio

3)jichanganye na watu tafuta fursa za kazi

4)usimpende kupitiliza jua ipo siku atakuacha au mtaachana usimgeuze ndio k**a mungu wako

5)akikufanyia tabia za uhuni mpotezee k**a umuoni yeye ndio ataumia akizani aumpendi

6) simu yake ione k**a ukoma ata ikiita usipokee usiwe na habari na simu yake

7)tafuta marafiki wazuri ambao unawaomba ushauri na wanakushauri vizuri

8)usiwe mtu wakuweka mambo moyoni jifunze kufurahi hata pasipo sababu Fanya furaha yako itokane na ww mwenyew

9)jipende, jijari,jiheshimu kuwa mtu bora usijiache ache usijizarau, usijichanganye na makundi ya ovyo

10)kila likufikalo omba DUA vita utaishinda na utaishi kwa furaha

NAKUPENDA SANA SHABIKI WANGU WA HII PAGEπŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™

Baba vijacho na mama vijacho mpo? Aya style za mishughuliko ndio hizo pindi wife akijaa kitumboπŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹
17/10/2022

Baba vijacho na mama vijacho mpo? Aya style za mishughuliko ndio hizo pindi wife akijaa kitumboπŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹

Address

Azizi Ally Uwanja Wa Sifa
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELIMU YA NDOA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ELIMU YA NDOA:

Share