Ndechi Inc

Ndechi Inc [email protected] Music website based in Tanzania. We post all new Hip-Hop/R&B tracks and videos. Follow us for daily updates.

Advertise/Inquiries To [email protected]

MJUE MJUSI (DINOSAUR) MKUBWA DUNIANI AMBAYE NI WETU(TANZANIA)Watu wengi hawajui kuhusu mjusi wetu, Leo tumfahamu vzuri. ...
21/10/2019

MJUE MJUSI (DINOSAUR) MKUBWA DUNIANI AMBAYE NI WETU(TANZANIA)

Watu wengi hawajui kuhusu mjusi wetu, Leo tumfahamu vzuri.
Kipindi cha ukoloni, Tanzania ilishawahi kuwa koloni la mjerumani, na katika kipindi hicho ndo mabaki ya mifupa ya mjusi wetu yaligunduliwa na wajerumani.

Mjusi wetu aligunduliwa mwaka 1907-1913 katika vilima vya Tendaguru mkoani Lindi na mgunduzi mjerumani aitwaye WERNER JANENSCH ambaye alikuwa mtaalamu wa mabaki ya wanyama.

Mjusi wetu alikuwa na mifupa zaidi ya 5000, yenye uzito wa tani 250 na hii imepelekea kutambulika na GUINNESS k**a mjusi mkubwa zaidi duniani kutokana na kuwa na urefu wa mita 13.27 (GUINNESS WORLD RECORDS). Baadaye uongozi wa kijerumani nchini uliamua kusafirisha ile mifupa kwende Berlin ujerumani mwaka 1909-1913 na kuhifadhiwa katika NATURKUNDEMUSEUM na imekuwa kivutuo kikubwa x**a kwa watalii na inawaingizia sana kipato ujerumani k**a chanzo chao cha utalii na hakuna hata shilllingi moja Tanzania tunapata ingawa ni Mali yetu(shamba la bibi)....!!!! *MSIMAMO WA SERIKALI* (Majadiliano bungeni bajeti 2016/2017)

mwaka 2016 wabunge walitaka mjusi huyu arudishwe. Majibu ya serikali yalikua k**a ifuatavyo; (1) Serikali ya Tanzania haina uwezo wa kiteknolojia kumtunza na makumbusho yetu hayana uwezo na vifaa vya kumtunza. (2) Njia nzuri ni kuongea na serikali ya Ujerumani kuona Tanzania itanufaikaje. (3) Serikali ya Ujerumani imekubali kuwasomesha watanzania watatu.

BARUA ALIYOANDIKA BILIONEA WA APPLE, STEVE JOBS KABLA YA KUFARIKI “Nilifikia kilele cha mafanikio katika biashara dunian...
18/10/2019

BARUA ALIYOANDIKA BILIONEA WA APPLE, STEVE JOBS KABLA YA KUFARIKI “Nilifikia kilele cha mafanikio katika biashara duniani. Katika macho ya watu wengine, maisha yangu ni kielelezo cha mafanikio. Hata hivyo, mbali na kufanya kazi, nina furaha ndogo. Kwa jumla, utajiri ni uhalisia tu wa maisha ambayo nimeyazoea.
Wakati huu ambao nimelala kitandani nikiwa mgonjwa na kuyakumbuka maisha yangu yote, ninagundua kwamba ufahamu utajiri nilionao umefifia kwa kuwa hauna maana wakati kifo kinakaribia.
Nikiwa gizani, ninautazama mwanga wa kijani kutoka katika mashine zinazonisaidia kuendelea kuishi na kusikia sauti za muungurumo wake, ninasikia na kuhisia pumzi za Mungu na za kifo zikinikaribia…
Sasa nafahamu kwamba tunapolimbikiza utajiri wa kutosha maishani mwetu, inatupasa kufuatilia mambo mengine ambayo hayahusiani na utajiri…
Kiwe ni kitu fulani ambacho ni muhimu zaidi:
Labda ni uhusiano, labda ni sanaa, labda ni ndoto inayoanzia katika siku za ujana…
Kutafuta utajiri muda wote utamwingiza mtu katika maisha yasiyofahamika, k**a mimi.
Mungu alitupa hisia za kutambua pendo katika kila moyo wa mtu, si mauzauza yanayoletwa na utajiri.
Utajiri nilioupata maishani mwangu siwezi kuondoka nao.
Ninachoweza kuondoka nacho ni kumbukumbu zilizojaa upendo.
Huo ndiyo utajiri wa kweli utakaokufuata, utakaoungana nawe, ukakupata nguvu na mwanga wa kusonga mbele.
Upendo unaweza kusafiri maelfu ya maili. Maisha hayana kikomo. Nenda unapotaka. Fika katika kilele unachotaka kufika. Yote yamo moyoni na mikononi mwako.
Ni kitanda gani chenye gharama zaidi duniani? Ni kitanda wanacholalia wagonjwa…
Unaweza kumwajiri mtu akaendesha gari lako, mtu akakuingizia fedha lakini huwezi kumpata mtu wa kubeba ugonjwa wako.
Vitu vilivyopotea vinaweza kupatikana. Lakini kuna kitu kimoja ambacho hakipatikani pindi kikipotea ni Maisha.

Mtu anapokwenda katika chumba cha upasuaji, atagundua kwamba kuna kitabu kimoja ambacho bado hajamaliza kukisoma “Kitabu cha Maisha ya Afya”.
Hata tukiwa katika daraja gani la maisha hivi sasa, muda ukifika, tutakabiliana na siku ambapo pazia la maisha litashuka.

Thamini Upendo kwa familia yako, mpende mwenza wako, marafiki zako. Jitambue vyema. MWISHO WA BARUA.!!

(SEHEMU YA KWANZA)HILI BOMU NDIO MFALME WA MABOMU YOTE KUWAHI KULIPULIWA ULIMWENGUNI, NDILO BOMU HATARI ZAIDI DUNIANI.Tu...
17/10/2019

(SEHEMU YA KWANZA)

HILI BOMU NDIO MFALME WA MABOMU YOTE KUWAHI KULIPULIWA ULIMWENGUNI, NDILO BOMU HATARI ZAIDI DUNIANI.

Tumekuwa tukisikia mabomu mabomu tokea tunaanza kujitambua hadi sasa , ila ni kwa mara chache tumepata kujiuliza uzito na uhatari wa mabomu hayo. Katika makala hii ninakuletea kiufupi bomu hatari zaidi kuwahi kutengenezwa na mikono ya mwana wa Adamu.
Mwanzoni mwa miaka ya 50 na 60 dunia ilishuhudia mpasuko mkubwa baina ya Mashariki na Magharibi, kipindi hiki ndio kilikuwa cha kupona vidonda baada ya kutoka kujeruhiwa na Vita kuu ya pili ya dunia, vita ambayo mtata Adolf Hi**er aliihenyesha dunia, vita ambayo kwangu mbabe huyu wa Kijerumani ninampa "credit" kwa kuionyesha dunia umahiri wake na commitment yake aliyokuwa ameiweka ili kuifanya Ujerumani kuwa super power duniani. Baada ya Ujerumani kuangushwa katika vita hii mataifa ya Marekani na Urusi kwa upande mwingine yaliwagombania wataalamu na Wanasayansi wa Ujerumani na kuwamishia katika nchi zao ili wakahamishie utaalamu wao katika nchi zao. Oparesheni hii ilipewa jina maarufu la "PAPERCLIP". Katika oparesheni hii Marekani iliwakusanya wataalamu, wahandisi na wanasayansi zaidi ya 1600 wa Kijerumani na Urusi pia iliwachukua wengi k**a mwenzake marekani.
Katika Mkutano mkuu wa umoja wa mataifa (United Nations General Assemby) wa mwaka 1960, Rais wa Urusi kipindi hicho bwana NIKITA KHRUSHCHEV aliikemea Marekani kwa maneno makali na kuahidi kuwaonyesha kuwa Urusi ni nani. Baada ya ahadi hiyo Bomu zito la TSAR BOMBA lilianza kuzaliwa katika mawazo ya wanafizikia wa Kirusi waliokuwa kwa wingi wamechukuliwa kutoka Ujerumani baada ya kuanguka kwa utawala wa Hi**er pamoja na wanasayansi wenyeji wa Urusi walianza kazi maabara ya kuzalisha kitu cha aina yake duniani.
Bomu hili liliandaliwa kuwa likilipuka litoe mlipuko wa uzito wa Megatoni (Tani Millioni) 100 lakini baada ya kukamilika liliweza kulipuka katika na kutoa mlipuko wa uzito kiasi cha Tani millioni 50, watalaamu wanasema k**a lingeweza kuachiwa kulipuka kwa intensity ya tani milioni 100 basi lingeweza kuipasua dunia katika vipande viwili mithili ya yai na hivyo kuiathiri hata Urusi yenyewe.
INAENDELEA..!!!
Like page yetu kwa kubonyeza kitufe cha like ili upate sehemu inayofuata.

26/08/2019

Waraka wa James Obedi

Afrika kwa sasa inashuhudia aina mpya ya utumwa kupitia Ukristo ikitwa *ulokole*.
Aina hii ya utumwa wa imani imewafanya watu wengi kuwa wavivu wa kufikiri na uwezo wa kutafakari mambo umedumazwa.

Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu. Wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa. Wanajitukuza wao zaidi kuliko kumtukuza yule wanayemhubiri.....Yesu Kristo.

Wachungaji wa aina hii hawawezi kuongelea mafanikio ya watu weusi k**a Barack Obama, Serena Williams, na Usain Bolt. Hawawezi kuongelea wagunduzi waliosaidia ku-transform dunia k**a kina Albert Einstein, Steve Jobs na wengine. Hawawezi kuongelea Wanasayansi walio-dedicate maisha yao na wengine kufia maabara wakitafuta dawa za kutibu magonjwa mbalimbali yanayoisumbua Afrika.

Hawawezi kuongea kuhusu wanafasihi vijana k**a Chimamanda Ngozi na Ben Okri, au wanafasihi wakongwe k**a Chinua Achebe na Ngugi wa Thiong'o.

Kila pembe ya dunia kuna watu waliofanikiwa kutokana na maarifa, bidii, ubunifu, na weledi. Wapo wafanyabiashara, wanasiasa, wanafasihi na hata wanasayansi wanaofanya mambo makubwa ya kuisaidia dunia yetu. Lakini wachungaji wa Afrika hawatawaongelea watu wa aina hii.

Wao wataongelea mtu aliyepata kazi kimiujiza licha ya kukosa sifa za kupata kazi hiyo, kwa sababu tu aliombewa na kupewa mafuta ya upako siku ya interview ya kazi.

Wataongelea kuhusu kijana aliyetoa mshahara wake wote kwa miezi mitatu mfululizo kwa Mchungaji wake k**a mbegu ya mafanikio, baadae akawa 'Boss' kazini.

Au wataongelea kuhusu kijana aliyefeli sekondari lakini baada ya baba yake kumalizia ukarabati wa nyumba ya Mchungaji, alipokea barua ya kupata 'admission' chuo kikuu bila hata kurudia mitihani.

Wachungaji hawa hutumia 'miujiza na shuhuda feki' k**a njia ya kuwafumba akili wafuasi wao. Kule Afika kusini kuna Mchungaji alidanganya kufufua mtu. Hata alipoomba msamaha baadae, bado kuna waumini wanaendelea kumuamini na kumsujudu.

Na wamegundua haya ndio mahubiri yanayopendwa sana huku Afrika. Hawataki kuhubiri kuhusu Aliko Dangote alivyoanza biashara na magumu aliyopitia mpaka mafanikio aliyopo sasa.

Wanahubiri kuhusu mama Janeth aliyekua mama Ntilie huko Enugu, lakini alipotumia mtaji wake wote wa shilingi laki 5 kununua mafuta ya upako kutoka kwa nabii fulani, ghafla biashara yake ikakua na sasa anamiliki mahoteli makubwa pande zote za nchi. Yaani bila mtaji, bila business plan, bila timeline ghafla tu akamiliki mahoteli. Na waumini watashangilia kwa sauti na kuitikia kwa kusema ameeeen.

Aina hii ya ukristo imepanda mbegu ya uvivu wa kufikiri kwa vijana wengi wa Afrika ambao wanalazimishwa kumuona Mungu k**a Mfadhili wa wavivu, au wasiostahili. Kwamba mwanafunzi hata asiposoma anajua akipewa mafuta ya upako atafaulu tu siku ya mtihani. Mfanyabiashara hata asipokua mbunifu anajua akienda kwa 'baba wa miujiza' biashara yake itapanuka ghafla bin vuu. Mfanyakazi hata asipowajibika kazini anajua akitoa fungu la kumi kwa 'Dokta Upako' atapanda cheo.

Kwa baadhi ya makanisa Afrika namna pekee ya kufanikiwa ni kufanya kile wanachokiita kupanda mbegu, kupaka mafuta ya upako au kunyunyuziwa maji ya baraka. Eti wanaofanikiwa haraka ni watu 30 wa mwazo wanaokimbilia mbele ya kanisa kila mmoja akiwa ameshika noti ya dola 100.

Aina hii ya mahubiri inawafanya watu waamini kwamba Mungu hawapendi wanaojituma na kuwa wabunifu katika kazi, badala yake anawapenda zaidi wanaotoa zaka, sadaka, malimbuko na fungu la 10 hata k**a ni wavivu. Hii sio sawa hata kidogo kwa sababu Biblia inakataa uvivu kwa nguvu zote (Mithali 12:27)
_
Watu wanaaminishwa kwamba ukishatoa sadaka kanisani unaweza kuamka kila siku asubuhi ukapayuka 'Mimi ni Milionea' halafu ukavuta shuka na kuendelea kulala fofofo, ukisubiri sadaka uliyotoa ikupe muujiza wa kuokota hela, ili upate mtaji wa biashara unayoiwaza.

Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive". Huu ni utani.

Waambieni wanaofanya huu utani kwa kofia za Uchungaji, Uaskofu, Unabii au Utume kwamba wanamkosea Mungu. Waambieni Mungu wetu ni Mungu wa kanuni, na hana kanuni ya kuwabariki wavivu. Tuache kufundisha waumini wetu kwamba uvivu unalipa kupitia miujiza.

Mafanikio ni matokeo ya bidii, ubunifu na weledi. Biblia inazungumzia kuhusu karama. Hebu kila mtu atumie karama alizopewa kwa bidii, ubunifu na weledi aone k**a hatafanikiwa. Sio sahihi kuwaambia watu wabweteke tu na kusubiria mafanikio k**a kusubiria daladala kituoni kwa sababu tu wamepakwa mafuta ya upako.

Mungu alishatubariki tangu wakati wa uumbaji wetu. Ni wajibu wetu kujibidisha katika yale tufanyayo ili baraka zake ziambatane nasi (Kumb 28:6).

Wazungu na Wachina wanazidi kushindana katika kuitawala dunia kwenye mambo mbalimbali kuanzia viwanda, biashara, sayansi na teknolojia. Sisi tuko 'busy' kununua maji ya upako tukiamini yatatufanya tuwe k**a Jack Ma au Bill Gates. Upuuzi.

Tumeumbwa kuitawala hii dunia (Mwanzo 1:28). Tutumie vipawa na karama tulizopewa ili kutimiza kusudi hilo la Mungu. Tusiruhusu Askofu, Mchungaji, Nabii, mtume au kiongozi mwingine yeyote wa dini atutawale akili zetu kwa kutuhubiria mafanikio ya miujiza. Wao wanashi kifahari kwa sadaka za waumini wao, huku waumini hao wakiendelea kuwa mafukara wa kutupwa.

Biblia inasema kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa (Mithali 1:7). Tutafute maarifa, tufanye kazi kwa bidii, na tumuabudu Mungu katika riho na kweli. Kwa kufanya hivyo tutapata MAFANIKIO katika mambo yote tuyafanyayo. Mungu akubariki unayesoma ujumbe huu.

by
James Obedi

Beijing Daxing International Airport inaanza kutumika Sept 30. Itakuwa moja ya airport kubwa Duniani, yenye uwezo wa kup...
15/08/2019

Beijing Daxing International Airport inaanza kutumika Sept 30. Itakuwa moja ya airport kubwa Duniani, yenye uwezo wa kupokea wasafiri 72m kwa mwaka na mizigo ya kufikia tani milioni 4. Itakuwa na runway 4 na terminal ukubwa wa viwanja 97 vya mpira!! ————————————————————————————ikianza kutumika hii, Jiji la Beijing, China litakuwa na viwanja viwili vikubwa. Yani jiji moja lenye ‘two world largest international airports’! Airport iliopo sasa imezidiwa inapokea wasafiri karibia 100m kwa mwaka!
———————————————————————————

Warusi ndio walikuwa wakwanza kurusha vyombo Mars mwaka 1971. Hata hivyo vilifia huko——————————————————————————Uingereza...
11/08/2019

Warusi ndio walikuwa wakwanza kurusha vyombo Mars mwaka 1971. Hata hivyo vilifia huko
——————————————————————————Uingereza ilirusha chombo mwaka 2003 kikafia huko pia
——————————————————————————Marekani wamesharusha vyombo vinne kwenda Mars mpaka sasa. Vitatu vimeshafia huko kimebaki kimoja tu wanachokiita ‘’Curiosity”. Bahati nzuri vyote vilifanikiwa kutuma picha Duniani kabla ya kufa. Sasa wanajiandaa kurusha vyombo viwili zaidi ‘’ExoMars’’ na ‘’Mars 2020’’
——————————————————————————-Vyombo hivi ni gharama! chombo kimoja kinagharimu takribani Trilioni TSh 5.9 ($2.5B)
———————————————————————————
Kuna siku tutakutana na wenzetu? !! Niachie mtazamo wako kwenye comment section.
————————————-

Tarehe k**a ya leo miaka 50 iliyopita binadamu watatu;  Neil Armstrong, Buzz Aldrin na Michael Collins kutoka Marekani w...
11/08/2019

Tarehe k**a ya leo miaka 50 iliyopita binadamu watatu; Neil Armstrong, Buzz Aldrin na Michael Collins kutoka Marekani waliondoka Duniani kuelekea mwezini wakiwa hawana uhakika k**a watafanikiwa kurudi!
————————————————————————— Walitumia chombo kilichoitwa Apollo 11. Siku nne baadae, (tarehe 20) walifika mwezini na wawili kati yao; Armstrong and Aldrin wakawa binadamu wakwanza kukanyaga ardhi ya mwezini. Collins hakushuka nje ya chombo. Wote walifanikiwa kurudi Duniani ———————————————————————————Hivi na sie tutafikia hatua hiyo lini?
———————————————————————————
For technology update like ukurasa wetu hapo juu kwa kubonyeza kitufe cha like page.

11/08/2019

Peniela (story ya kijasusi)

SEASON 1
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI : PATRICK.CK
Ni saa sita za usiku sasa bado jaji Elibariki chukuswa yuko sebuleni akiendelea kupitia kitabu chake cha sheria .Katika meza ndogo kulikuwa na vitabu vingine zaidi ya saba vya sheria.Aliendelea kufungua ukurasa baada ya ukurasa.Alionekana kuwa na mawazo mengi mno.Wakati akiendelea kupitia kurasa za kitabu kile mke wake akaingia pale sebuleni akiwa na kikombe cha kahawa, akakiweka mezani halafu akainama na kumbusu mumewe.

“ You need to take a rest now.Tommorow is your big day” akasema Flaviana mwanamke mwenye uzuri wa kipekee.Elibariki akakifunika kitabu chake na kumtazama mkewe ,akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kusema

“ Natamani sana nipumzike lakini sina hakika k**a nitapata usingizi.”
Mke wake akamuangalia kwa makini halafu akasema
“ Kuna jambo nataka nikuulize mume wangu”
“ Uliza usihofu ”
“ Najua kesi hii ni moja kati ya kesi kubwa na ngumu kwako.Hukumu unayotarajia kuitoa kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa sana na umma wa watanzania.Wewe ni jaji na nina imani maamuzi yako utakayoyachukua ni sahihi kabisa,lakini swali langu ni je Yule msichana ana hatia?
Swali lile lilionekana gumu sana kwa jaji Elibariki.Akainama akafikiri kidogo halafu akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kumtazama mkewe.

“ My love kesi hii ni ngumu sana na imejaa utata mwingi na ndiyo maana unaniona mpaka hivi sasa bado niko hapa.” Akasema Elibariki
Flaviana akamtazama mume wake na akagundua kwamba hakuwa tayari kumjibu swali alilouliza.Akas
imama na kusema

“ Sina wasi wasi na maamuzi utakayoyatoa kesho lakini nakuomba utoe haki kwa upande wenye haki.”
Elibariki hakumjibu kitu akabaki akimuangalia
“ Come to bed when you are done,but don’t stay till very late.You have a big day tomorrow.” Akasema Flaviana na kuelekea chumbani .Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuchukua kitabu chake cha sheria akaendelea kukisoma.
“ Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na kesi ngumu yenye mitihani k**a hii.Hata hivyo niliapa kusimamia sheria na kutenda haki kwa kila mwenye haki.

Katika maamuzi yangu ya kesho lazima nifanye kwa haki japokuwa nina hakika nitakuwa katika matatizo makubwa baada ya hukumu ya kesho lakini siwezi kupindisha sheria eti tu kwa sababu ya shinikizo toka kwa mtu au kikundi cha watu.Mungu ataniongoza na kunisimamia ili nitoe hukumu ya haki” akawaza Elibariki na kufunga vitabu vyake akaelekea chumbani kulala.tayari Flaviana mke wake amekwisha lala.Akamtazama kwa makini na kujisemea moyoni

“ Nina hakika hata wewe hautanitazama vizuri baada ya hukumu ya kesho,lakini sina namna nyingine zaidi ya kutenda haki.Utanisamehe mke wangu” akawaza Elibariki na kupanda kitandani kulala.

***********

“ Eli my love,amka kumekucha !! ..Ilikuwa ni sauti tamu na laini ya Flaviana akimuamsha mumewe.Jaji Elibariki ambaye asubuhi hii alionekana kuzama katika usingizi mzito akafumbua macho huku akiguna na kutazama saa ya ukutani.Ni saa kumi na mbili na dakika ishirini za asubuhi.
“ jana sikupata usingizi kabisa.Usiku wangu ulikuwa mrefu sana” akasema kwa sauti ya uchovu.

“ Please wake up honey.Today its going to be a very long day” akasema Flaviana.Elibariki akainuka na kuelekea katika chumba chake cha mazoezi akafanya mazoezi kidogo halafu akaelekea bafuni.Bado kichwa chake kiliendelea kuwa na mawazo mengi sana.Kisha oga akarejea chumbani na kukutana na suti nzuri aliyoandaliwa na mke wake akavaa na kujitazama katika kioo kikubwa kilichokuwamo chumbani mwao.Aliganda pale katika kioo hadi mke wake alipoingia naye akaanza kujiandaa.

“ Leo unakwenda kazini? Akauliza Jaji Elibariki.Flaviana akacheka kidogo na kusema
“ Usinichekeshe mume wangu,yaani niende kazini leo? Siwezi kufanya hivyo hata kidogo.Leo ni siku yako kubwa.Ni siku yetu kubwa.Ni siku ambayo jina lako litaingia katika vitabu vya historia kwa hukumu unayokwenda kuitoa.Vyombo vyote vya habari vitakuwepo mahak**ani ,lazima na mimi niwepo nikuunge mkono pamoja na mdogo wangu Anna.” Akasema Flaviana.Elibariki hakujibu kitu akaendelea kujitazama katika kioo.

“Are you nervous my love? Akauliza Flaviana
“ No I’m not” akajibu Elibariki halafu wakaongozana kuelekea katika chumba cha chakula kwa ajili yakupata kifungua kinywa.Wakati wakiendelea na kupata kifungua kinywa simu ya Jaji Elibariki ikaita.Akaitazama ikiita akasita kuipokea.
“ Mbona hupokei hiyo simu? Akauliza Flaviana
“ Its your father.Mr President” akajibu Elibariki
“ Usiogope.Ongea naye .Si kawaida yake kupiga simu mida k**a hii.Inawezekana ana jambo la maana la kukwambia” Akasema Flaviana.Elibariki akaichukua simu na kubonyeza kitufe cha kupokelea huku akiinuka na kuelekea sebuleni.

“ Hallo Mr President” akasema Jaji Elibarki
“ Hallo Jaji.Mnaendeleaje vijana wangu?
“ Tunaendelea vizuri mzee.Ninyi mnaendeleaje?
“ Tunaendelea vizuri sana”
“ Nashukuru kusikia hivyo” akasema Elibariki na kimya kifupi kikapita
“ Elibariki,today its your big day” akasema Mheshimiwa rais.
“ Najua unakwenda kutoa hukumu katika kesi ngumu inayovuta hisia za watu wengi na hasa kwa kuwa binti wa rais naye kesi hii inamuhusu kwani mchumba wake ndiye aliyeuawa.Sikufundishi kuifanya kazi yako lakini fanya maamuzi ya haki kwa namna uonavyo wewe.Pamoja na hayo kuna jambo ambalo nataka kukuomba kijana wangu” Akasema Dr Joshua Johakim rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“ Nakusikiliza mzee” akasema Jaji Elibariki kwa wasi wasi .
“ Nilikuteua kuwa jaji kwa sababu wewe ni msomi mzuri na unazifahamu sheria za nchi kwa hiyo sitaki kuingilia maamuzi yako lakini nakuomba kijana wangu,try in anyway you can to make my daughter Happy.Alimpenda sana Edson.Ni hilo tu ninalotaka kukuomba kijana wangu.Nakutakia siku njema” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alibaki ameduwaa asijue afanye nini.Maneno yale ya rais ambaye ni baba mkwe wake yalimfanya ahisi kuchanganyikiwa.

“ Huu ni mtihani mgumu sana lakini Mungu atanitangulia nitatenda haki” akawaza Elibariki na kurejea mezani
“ Amekwambia nini baba? Mbona sura yako imebadilika namna hiyo? Akauliza Flaviana
“ Nothing.Just greetings” akajibu Elibariki na kuendelea kupata kifungua kinywa.Baada ya kumaliza akarejea chumbani na kujitazama tena katika kioo na kuvuta pumzi ndefu.

“ Please help me Lord.I’m in a very difficult situation” akasema Elibariki kwa sauti ndogo na mara mke wake akaingia mle chumbani
“ Its time my love.Are you ready?
“ Let’s go” akasema Elibariki ,wakatoka wakaingia garibni na kuondoka.

**********

Hakukuwa na nafasi tena ya kukaa ndani ya chumba cha mahak**a kutokana na watu kujaa.Ni siku ya hukumu ya kesi ya mauaji inayomkabili mmiliki wa maduka makubwa ya mavazi ya Penny Fashion,Peniela Salimote.Kesi hii iliyovuta hisia za watu wengi na kuwafanya wafurike ili kuja kusikia hukumu ilikuwa inaonyeshwa moja kwa moja katika runinga.ILikuwa ni kesi ya kwanza kubwa kurushwa moja kwa moja katika runinga.Katika kila kona ya nchi watu walikuwa wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja ya kesi hii ambayo hukumu yake ilikuwa inasubiriwa na watu wengi.

Ndani ya chumba cha mahak**a ilikuwepo familia ya rais ikiongozwa na mke wa rais,Dr Flora Johakim ambaye alikuwa ameambatana na binti zake wawili Flaviana na Anna.Familia ya Edson Kobe kijana anayedaiwa kuuliwa na Peniela nayo ilikuwepo mahak**ani hapo ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.Familia ya Edson na ile ya rais zilikuwa ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Kwa upande wa Penny hakukuwa na ndugu yake yeyote aliyefika mahak**ani pale zaidi ya rafiki zake wachache.

Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahak**ani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake .
“ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.

“ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia.Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Najua chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka
“ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakikisha kwamba tunashinda kesi hii lakini k**a mambo yataenda tofauti na matarajio yetu hautakuwa ni mwisho.Nitapambana hadi nihakikishe haki imepatikana.” Akasema Jason na mara jaji akaingia.

Wakati Jaji akiingia Penny akamnong’oneza Jason sikioni
“ I didn’t do it.I didn’t kill him”
“ I know Penny and I believe you” akasema Jason na mara mahak**a ikaanza.”

Hizi ndizo nyumba ambazo NASA wameridhia zikajengwe kwenye sayari ya Mirithi (mars).,......................................
29/07/2019

Hizi ndizo nyumba ambazo NASA wameridhia zikajengwe kwenye sayari ya Mirithi (mars).
,............................................................................
Mwaka 2015 NASA walitangaza shindano kwa watu/kampuni kutengeneza nyumba za 3D kupitia nyenzo zinazopatikana kwenye sayari ya Mirithi. Na hizo nyumba ndefu pichani ndizo ambazo NASA waliridhia. Mirithi ndiyo sayari pekee kwenye mfumo wetu wa Jua ambayo inafanana na Dunia, na tayari kampuni ya Space X wanampango wa kupeleka watu 2024 na ikiwezekana kutengeneza jiji ambalo watu watakuwa wanaishi ifikapo mwaka 2050.

Address

Chekereni Alongside Munio Headquarters
Dar Es Salam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 22:00
Thursday 09:00 - 22:00
Friday 09:00 - 22:00
Saturday 09:00 - 22:00

Telephone

0659520960

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ndechi Inc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Ndechi Inc:

Share