Simulizi Za John Njelekela

Simulizi Za John Njelekela Kurasa huu ni wa simulizi tu, nyote nawakalibisha

Kitabu cha Kifo kinazindua kitabu kipya ambacho nikitabu cha kwanza kabisa kuzinduliwa kupitia kitabu hichi cha Kifo...BORA NIFE, Bora nife nikitabu cha simulizi kilichotungwa na mtunzi nchini John simon njelekela. Kitabu hichi kinamzungumzia Baba mmoja kutokea pande za Mwanza, pia mwandishi wa kitabu hichi amejalibu kutoa maelezo mazuri ambayo yatamfanya msomaji kuelewa vizuri. 0757215595 Hizi ni

namba za mwandishi wa kitabu hichi ambaye anapatikana maeneo ya Shinyanga, KATIKA kitabu ichi utapata kuona ni jinsi gani Mustafa alivyo fanyiwa kitendo cha ukatili na Binadamu wenye roho mbaya roho ya kishetani..Ndugu zangu na waomba mjalibu warau kukifatilia kitabu hicho ilimuweze kujifunza katika maisha ya kila siku...

13/05/2023

Hadithi Ya Kweli ...MVUVI

Mwandishi ...John Njelekela

WhatsApp ....0747838773

Sehemu ya {01}

Ilikuwa tarehe 6_6_2006, Saa 12:30 jioni ndege na milio ya wadudu mbalimbali ilikuwa ikitawala katika kisiwa kidogo kinachopatikana katika ziwa Victoria maharufu k**a kisiwa cha Saa 8 kipatikanacho hapo jijini Mwanza, lakini hapakuwa na ndege wala wadudu pekee bali kulitawaliwa na wavuvi ambao walikuwa wakazi wa kisiwa hicho cha Saa8
"Oya, zana zote zimeingia kwenye mtumbwi?" ..
" Mustapha Unga tayari umeshaingiza na vyombo k**a bado hakikisheni kuwa vimo ndani ya mtumbwi"...
"Sawa kiongozi, Omary Njoo unisaidie kubeba hii Nyavu".....
Yalikuwa ni baadhi ya mazungumzo ya wavuvi hao ambao walikuwa katika furaha kubwa sana na kila mmoja wao alikuwa akitabasamu kuonyesha furaha kubwa na upendo wakweli utokao ndani ya myoyo yao. Katika kundi hilo la wavuvi basi kulikuwa na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la David ,David alikuwa nikija aliyebarikiwa kwani sifa yake kuu ilikuwa ni kwamba akitega samaki nyavuyake uk**ata samaki zaidi 1000 kwa dakika chache tu hivyo basi kutokana na sifa aliyokuwanayo iliwafanya watu kuwa na wivu juu yake haswa wavuvi wenzake, hii siku alikuwa ameketi juu ya Mtumbwi mkono wake wakulia akiwa ameshika Embe taratibu akaliuma kidogo kisha akampatia nayule aliyekuwa ameketi jirani yake na baada ya maandalizi yote kukamilika basi wakajikita ndani ya Mtumbwi kwa safari ya kwenda katikati ya ziwa kuwatega samaki. Maisha ya Uvuvi yalimpa uthamani mkubwa sana Davi kwani kupitia pesa alizokuwa akizipata alikuwa akiwalipia Ada ya shule wadogo zake wawili japo kaka yake mkubwa ambaye yu katika Uvuvi akipata fedha basi uishia vilabuni na kuhonga wanawake tofauti tofauti , miezi kadha iliyopita walimpoteza Baba yao Mama yao nae anasumbuliwa na Kifua kikuu .Tegemezi lilibaki kwa David na Kaka yake Andrew ,Japo Andrew alikuwa kwisha oa mwanamke ambaye waliamini yakuwa ndie mwangalizi wa Mama yao pale wanapokuwa katika shughuli zao za Uvuvi lakini hai kuwa hivyo mateso na Manyanyaso yalikuwa yakimkumba Mama yao mzazi .
Ingawa Julieth kuyaweka adharani mapenzi yake kwa kuamua kumzalia Andrew mtoto mmoja wa kiume aliyepewa jina la Babu yake yaani Baba yake Andrew alifahamika kwa jina la Abdnego ,hii ndiyo ilikuwa familia ya Andrew na mkewe Julieth japo mdogo wake ndio kwake yu katika Mahusiano na Isabella na muda si mrefu Davi alienda kwao Isabella kujitambulisha .Kitendo cha Davi kutaka kuoa hakikumfurahisha Shemeji yake kwani aliamini kuwa hatoishi kwa amani pale Isabella atakapo kuja kuishi karibu nae.
"Haiwezekani ,yaani k**a ameshindwa kumzuia mdogo wake asioe basi mimi tabeba mwanangu na kuondoka hapa, atakuwa amenichoka sasa"
Yalikuwa ni mawazo ya Julieth juu ya Mume wake kushindwa kumzuia Davi katika swala zima la kuoa .Hata walipo rejea kutoka kazini hii siku Andrew akunywa pombe kabisa hii ikawa njia pekee ya mkewe kumshauri jambo la kufanya juu ya Davi.
"Mume wangu , hivi umekaa tu kimya k**a unipendi na k**a umenichoka si uniambie tu ukweli ili nijue"
"Mke wangu mbona sikuelewi unamaanisha nini kusema hivyo?"
"Unajifanya ujui eti?"
"Ndio sijui, ningelijua ningekuuliza mke wangu"
"Hivi unataka hii Nymarehemu Nyumba ya kulelea watu, haujui k**a Davi hicho kikaragosi chake kitakuja kukuharibia maisha yako ?"
"Kivipi atayaharibu maisha yangu pia tambua yakuwa mdogo wangu kwisha fikisha umri wa kuoa na awezi kwenda kuishi sehemu nyingine tofauti na hapa ,na marehemu Baba yetu alitukabidhi Nyumba hii tuishi na Mama tumtunze vizuri ".
" Haaaah!, kweli Siku zote nakuambia wewe ni mwanaume jina tu".
Majibu ya Julieth yalizidi kumweka hatiani Andrew aliwaza sana pale alipo mtazama mkewe akitokwa na machozi kwa kitendo tu cha shemeji take kuoa.
"Sina jinsi wala namna nitafanya k**a atakavyo ili niulizishe moyo wake".
Yalikuwa ni mawazo ya Andrew na kweli siku iliyofuata baada ya kutoka katika mihangaiko yao ya uvuvi , Usiku wakiwa chumbani alimuuliza mkewe....
" Nipo tayari kufanya lolote lile mke wangu ilitu mdogo wangu asioe, haya niambie nifanye nini sasa?".
"Aaaah, ndo maana nakupenda kila kukicha upendo unazidi kuongezeka dhidi yako, Chakufanya Mume wangu Muuwe tu ili asije kutusumbua mbeleni harafu Mali zote utazimiliki peke yako".
Lili kuwa wazo la Julieth kwa Mumewe japo Mumewe akulipokea kwa furaha lakini maneno matamu yaliyo toka katika kimya cha Julieth mkewe yalizidi kumshawishi hatimaye akakubali kumua Davi................

Itaendelea

Njoo WhatsApp 0747838773

17/02/2021

Habari njema kwako mtanzania ,unakipaji cha uandishi wa fasihi yaani Riwaya pamoja na Tamthilia k**a unakipaji basi jiunge nasi katika udumishaji wa kazi za fasihi kwa ujumla
Asante

08/01/2021

SIMULIZI YA NASRATI (kiumbe wa AJABU) 📖

Mtunzi....JOHN NJELEKELA

Whatsapp 0747838773

Epsod 1

SONGANAYO.....

✏️Sauti za ajabu zilisika ngurumo na ndelemo nazo zilishahimili kwa kiasi kikubwa hata katika nyumba ndogo ya mzee Chawele zilisikika kwa kiasi kikubwa kilichopekea kukosa usingizi kwa kijana mdogo aitwaye George, hali hii ilikuwa ikimsumbua sana hasa nyakati za usiku George alizidi kulalamika uku akiomba msaada
" Mama nisaidie nakufa...Mamaaa"
alipiga kelele za msaada uku akifurukuta na kurusha miguu uku na kule, kutokana na ukaribu wa vyumba kati George na wazazi wake ilipelekea kusikika kwa sauti ile hivyo upesi Chawele na mke Sindua, wakaamka chakwanza kabla ya yote Chawele akalivuta panga lake chini ya kitanda upande wa Sindua akanyanyua vyema kipande cha tofali ,Chawele akamsogelea mkewe na kumnong'oneza kitu
"natangulia mimi endapo watakuwa majambazi basi nitawafyeka vibaya mno"
"wakiwa ni watu wa baya basi pande hili la tofali litakuwa halali yao na sivinginevyo"
ilikuwa sauti ya minong'ono kati ya wawili hawa , walifungua mlango na taratibu kwa mwendo wa kunyata wakausogelea ule mlango wa chumba alichokuwa amelala George, kwa kuwa mlango ulikuwa wa kuegeshwa kutokana na hali duni waliyokuwa nayo ya kushindwa kununua mlango wa kisasa hivyo awakupata shida kuingia ndani mle. Sindua akavuta pumzi kwa mashambulizi yatakayo jitokeza akaunyanyua mkono wa kulia uliyoshika jabali vyema kabisa uku mkono wa kushoto akiwa ameik**ata tochi kwa lengo moja tu pale Chawele mumewe atakapo ufungua mlango basi ammulike tochi adui ilikumzubaisha, kweli mambo yakawa shwari k**a walivyo panga wawili awa na baada ya Chawele kuufungua mlango kwa shahuku ya kutaka kujua kilichomkumba mwanae ndipo mwanga hafifu ukatanda katika chumba kile hii ilitokana na tochi iliyowashwa na mkewe Sindua.
"George , wee George"
Chawele alizidi kumwita mwanae uku akijalibu kumtingisha tingisha.
"aaaa na...ku.."
alizungumza George kisha ukimya ukamtawala kwa muda, sekunde kadhaa fahamu zikamrejea japo alikuwa akihema kwa nguvu hali hii ilimuonyesha kuwa na wasiwasi sana.
Baada tu ya kupambazuka safari ilianza ambayo lengo kuu ni kwenda kwa mtaalamu yaani mganga wa kienyeji ambaye waliamini fika kwamba atakuwa msaada mkubwa kwa kijana George, Baada ya kufika kwa Mganga aliyeaminika pale kijini hawakupata shida ya kujieleza kwani tunguli za mganga zilijizihilisha vyema .
''Aaaaaahhh,eeeh!!! Mizimu kutoka Mashariki ,Magharibi na Kusini ..Tawile eeh!!!!,,.
Zilikuwa ni mbwembwe za Mganga maarufu Kamchape zilizozidi kutamba katika kizimba chake kilichopo kando ya kijiji hicho kilichojulikana kwa jina k**a Mfiringe.

''Aaaah, Mimi ndiye Kamchape Mganga nae ogopeka kote ulimwenguni ..eeehh!! Kijana wenu anasumbuliwa na tatizo kubwa sana ..Ndio tatizo kubwa na hatakapo fikisha umri wa miaka 18 ataitajika katika ufalme wa Majini na hicho ndicho kihapo alichokipokea'''

''Kosaaa!!!kosa gani hilo na kihapo gani alichokipokea mwanetu?''

''Sina majibu ya kuwapa kazi yangu nimeshaimaliza , siwezi kuingilia mambo mazito k**a haya ,nawasihi ondokeni haraka sana''

Chawele na mkewe Sindua wakiwa sambamba na George waliondoka eneo lile kulingana na maelezo ya mganga hivyo upesi waliti agizo .Wakiwa njiani Chawele alimuuliza mkewe...
''Mke wangu hii hali ya mwanetu itaendelea mpaka lini maana kila kukicha hali inazidi kuwa mbaya sana , tufanye nini tena?''.
" Mume wangu kwanini tusimuondoe hapa kijiji tumpeleke kwa Mama take Mdogo jijini Mwanza"
"Mh nalo nineno mke wangu nahisi wanamchezea hapa kijijini".
Yalikuwa ni mazungumzo kati ya Sindua na Mume Chewele.

KOSA KUBWA BILA KUJUA

Ndugu msomaji ni heri shali kulikolile lijalo na k**a wangelijua wasingemwamisha pale kijijini kitendo cha George kupelekwa Mwanza kilimfanya kuwa George wa aina yake anakumbana na misuko suko ya kulazimishwa afunge ndoa na binti Nasrati kutoka katika ufalme wa Majini ..

Itaendelea

Njoo WhatsApp 0747838773

19/02/2020
https://chat.whatsapp.com/DwEEjTdexzC2NTlzgN60hB
12/01/2020

https://chat.whatsapp.com/DwEEjTdexzC2NTlzgN60hB

WhatsApp Messenger: More than 1 billion people in over 180 countries use WhatsApp to stay in touch with friends and family, anytime and anywhere. WhatsApp is free and offers simple, secure, reliable messaging and calling, available on phones all over the world.

13/12/2019

ambapo waliyaanza maisha yao mapya kwa kuishi katika nyumba za kupanga uku Zuhena akiendeleza kimradi chake cha kuuza bidhaa ndogo ndogo katika magenge hapo mkoani Tanga, katika upande wa Subira aliendelea na masomo yake katika shule ya Mwembeni iliyoko hapo mkoani Tanga. Kutokana na sheria za uhamiaji katika shule hiyo ilimlazimu kurudia darasa la sita ilikuyazoea mazingira ya shule kabla ya kukabiliana na mtihani wa Taifa wa darasa la Saba, Subira akaendelea na masomo kutokana na uelewa wake wakaribu ulimfanya kuwa maarufu sana pale shuleni kitendo ambacho kilimfanya ajibebe sifa tele kutoka kwa walimu na wanafunzi wenzake na hatimaye baada ya miaka miwili anafanikiwa kumaliza elimu ya msingi na kubahati kuchaguliwa kuwa mwanafunzi bora aliyefanya vizuri katika somo la hisabati. Serikali mlimtazama Subira kwa jicho la tatu akiwa katika elimu ya sekondari , Zuhena mamae Subira alijitaidi kadri awezavyo kupata fedha kwa ajili ya kutimiza ndoto za mwanae Subira

13/12/2019

"Baba Subira, wee ni mtu wa pombe tu kila kukicha uoni hata haya jamani?" . "wee nani haswa hadi unifundishe maisha....", sauti ya ulevi ilizidi kumtoka Matatizo kupelekea hadi kumpiga mkewe ya bila sababu yoyote ile. "Jamani msaada nakufa mimi" Zuhena mkewe Matatizo alilalamika kutokana na kipigo kikali alichokumbananacho kutoka kwa Mumewe Matatizo. "Mamaaa....", ilikuwa ni sauti ya Subira ikimlilia Mama yake, " WEWE BABA SUBIRA UTAMUA MKEO, VUTA UKU TUMTOE". Zilikuwa ni sauti za majira baada ya kusikia mtafaruko wa nyumba hiyo na sauti ya msaada iliyotolewa wa Zuhena. Kiukweli Zuhena alijiapiza waziwazi kuvunja mahusiano yao na baada ya ugomvi ule kutokea akuweza kuishi na mumewe baada ya mwenyekiti wa kijiji kuharalisha mvunjiko wa ndoa yao na hatimaye kutokomea Mheza Mkoani Tanga

10/12/2019

"Eeeh Mungu nimekosa nini mimi Matatizo ingawa jasiri na mwenyenguvu.. wewe mwanamke fungua jembe liingie unajifanya kibuli sana mimi ndie k**anda ..aaaah!." Alizungumza kwa sauti ya juu ambayo hata majira zake ziliwashtua pia lakini kutokana na hali zoelefu ya ulevi walikuwa kwisha mzoea, akiwa nje ya mlango alianza kupiga mateke mlango kitendo hicho kilipelekea mkewe kushtuka simkewe tu hata mwanae Subira aliweza kuamka kutoka usingizini

27/11/2019

benson akiwa katikati ya jiji alibofya kitufe flani kilicho kuwa ndani ya gari lake baada ya kubofya kitufe hicho vioo vikafunguka na ndipo benson akamulikwa na mwanga hafifu ambao ulisababisha aonekane na kila mtu hasa kwa wale waliokuwa wakitembea kwa miguu , kitendo cha kuoneka na kila aliyemtazama kilimfanya ajione ye nibora zaidi katika Dunia hii hasa alivyo itazama suti yake nadhifu hapo ndipo akaweka tumaini moyo mwake akuna mrembo yeyote yule anayeweza kukatiza mbele yake ya bila kudondosha mate ya matamanio. Naam! baada ya muda kadhaa safari yake ikafika ukomo akashuka garini kwa madaha ya aina yake akafunga mlango wa gari kwa kutumia miguu yake kisha ndipo aka lock kwa kutumia remote ya ilikuwa imefungwa katika funguo za gari lake, moja kwa moja Benson akaelekea katika jengo flani hivi lililo pambwa kwa maua mbalimbali na kuchukua nafasi katika Marashi ya aina yake .,Ndio! Manukato nayo yaliongeza uzuri kwa kiasi chake.

"Niko wapi hapa sasa"  , nilijiuliza maswali na muda uo uo ghafra nikavutwa na mtu ambaye nilikuwa simfahamu bali alikuw...
15/09/2019

"Niko wapi hapa sasa" , nilijiuliza maswali na muda uo uo ghafra nikavutwa na mtu ambaye nilikuwa simfahamu bali alikuwa yu msicha pia alikuwa amevalia mavazi meupe na chini alikuwa amevaa viatu vyekundu bila kusahau alikuwa na nywele ndefu kichwani. Baada ya kunivuta kwa nguvu nikawa nimesogea usawa kabisa na watu wale waliokuwa wakicheza ngoma,, nikiwa nimebaki bumbuwazi ghafra nikapewa maji ya kunywa na kwa kuwa nilikuwa na kiu isiyo koma upesi upesi nikapokea maji yale kisha nikayanywa; Masaa kadhaa kupiti baada ya kunywa maji yale kutoka kwa watu ambao nilikuwa siwafahamu.... Upepo mwanana unanipuliza , taratibu nayafumbua macho yangu mwanga hafifu unatokea machoni mwangu kwambali sauti inasikika ikiniita.."Igodo amka " ,,,," Nasema niacheniiiii" nilipiga kelele ambayo ilinifanya nishtuke kwanguvu ; Naam baada ya kushtuka kundi la watu wakinishangaa wakiwemo wanafunzi wenzangu .
" Jamani uyu mtoto tokea alale hapa ni muda umepita zaidi" baadhi ya watu wale walio kuwa wakinishangaa walikuwa wakizungumza

04/09/2019

Address

Maswa

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi Za John Njelekela posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category