13/05/2023
Hadithi Ya Kweli ...MVUVI
Mwandishi ...John Njelekela
WhatsApp ....0747838773
Sehemu ya {01}
Ilikuwa tarehe 6_6_2006, Saa 12:30 jioni ndege na milio ya wadudu mbalimbali ilikuwa ikitawala katika kisiwa kidogo kinachopatikana katika ziwa Victoria maharufu k**a kisiwa cha Saa 8 kipatikanacho hapo jijini Mwanza, lakini hapakuwa na ndege wala wadudu pekee bali kulitawaliwa na wavuvi ambao walikuwa wakazi wa kisiwa hicho cha Saa8
"Oya, zana zote zimeingia kwenye mtumbwi?" ..
" Mustapha Unga tayari umeshaingiza na vyombo k**a bado hakikisheni kuwa vimo ndani ya mtumbwi"...
"Sawa kiongozi, Omary Njoo unisaidie kubeba hii Nyavu".....
Yalikuwa ni baadhi ya mazungumzo ya wavuvi hao ambao walikuwa katika furaha kubwa sana na kila mmoja wao alikuwa akitabasamu kuonyesha furaha kubwa na upendo wakweli utokao ndani ya myoyo yao. Katika kundi hilo la wavuvi basi kulikuwa na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la David ,David alikuwa nikija aliyebarikiwa kwani sifa yake kuu ilikuwa ni kwamba akitega samaki nyavuyake uk**ata samaki zaidi 1000 kwa dakika chache tu hivyo basi kutokana na sifa aliyokuwanayo iliwafanya watu kuwa na wivu juu yake haswa wavuvi wenzake, hii siku alikuwa ameketi juu ya Mtumbwi mkono wake wakulia akiwa ameshika Embe taratibu akaliuma kidogo kisha akampatia nayule aliyekuwa ameketi jirani yake na baada ya maandalizi yote kukamilika basi wakajikita ndani ya Mtumbwi kwa safari ya kwenda katikati ya ziwa kuwatega samaki. Maisha ya Uvuvi yalimpa uthamani mkubwa sana Davi kwani kupitia pesa alizokuwa akizipata alikuwa akiwalipia Ada ya shule wadogo zake wawili japo kaka yake mkubwa ambaye yu katika Uvuvi akipata fedha basi uishia vilabuni na kuhonga wanawake tofauti tofauti , miezi kadha iliyopita walimpoteza Baba yao Mama yao nae anasumbuliwa na Kifua kikuu .Tegemezi lilibaki kwa David na Kaka yake Andrew ,Japo Andrew alikuwa kwisha oa mwanamke ambaye waliamini yakuwa ndie mwangalizi wa Mama yao pale wanapokuwa katika shughuli zao za Uvuvi lakini hai kuwa hivyo mateso na Manyanyaso yalikuwa yakimkumba Mama yao mzazi .
Ingawa Julieth kuyaweka adharani mapenzi yake kwa kuamua kumzalia Andrew mtoto mmoja wa kiume aliyepewa jina la Babu yake yaani Baba yake Andrew alifahamika kwa jina la Abdnego ,hii ndiyo ilikuwa familia ya Andrew na mkewe Julieth japo mdogo wake ndio kwake yu katika Mahusiano na Isabella na muda si mrefu Davi alienda kwao Isabella kujitambulisha .Kitendo cha Davi kutaka kuoa hakikumfurahisha Shemeji yake kwani aliamini kuwa hatoishi kwa amani pale Isabella atakapo kuja kuishi karibu nae.
"Haiwezekani ,yaani k**a ameshindwa kumzuia mdogo wake asioe basi mimi tabeba mwanangu na kuondoka hapa, atakuwa amenichoka sasa"
Yalikuwa ni mawazo ya Julieth juu ya Mume wake kushindwa kumzuia Davi katika swala zima la kuoa .Hata walipo rejea kutoka kazini hii siku Andrew akunywa pombe kabisa hii ikawa njia pekee ya mkewe kumshauri jambo la kufanya juu ya Davi.
"Mume wangu , hivi umekaa tu kimya k**a unipendi na k**a umenichoka si uniambie tu ukweli ili nijue"
"Mke wangu mbona sikuelewi unamaanisha nini kusema hivyo?"
"Unajifanya ujui eti?"
"Ndio sijui, ningelijua ningekuuliza mke wangu"
"Hivi unataka hii Nymarehemu Nyumba ya kulelea watu, haujui k**a Davi hicho kikaragosi chake kitakuja kukuharibia maisha yako ?"
"Kivipi atayaharibu maisha yangu pia tambua yakuwa mdogo wangu kwisha fikisha umri wa kuoa na awezi kwenda kuishi sehemu nyingine tofauti na hapa ,na marehemu Baba yetu alitukabidhi Nyumba hii tuishi na Mama tumtunze vizuri ".
" Haaaah!, kweli Siku zote nakuambia wewe ni mwanaume jina tu".
Majibu ya Julieth yalizidi kumweka hatiani Andrew aliwaza sana pale alipo mtazama mkewe akitokwa na machozi kwa kitendo tu cha shemeji take kuoa.
"Sina jinsi wala namna nitafanya k**a atakavyo ili niulizishe moyo wake".
Yalikuwa ni mawazo ya Andrew na kweli siku iliyofuata baada ya kutoka katika mihangaiko yao ya uvuvi , Usiku wakiwa chumbani alimuuliza mkewe....
" Nipo tayari kufanya lolote lile mke wangu ilitu mdogo wangu asioe, haya niambie nifanye nini sasa?".
"Aaaah, ndo maana nakupenda kila kukicha upendo unazidi kuongezeka dhidi yako, Chakufanya Mume wangu Muuwe tu ili asije kutusumbua mbeleni harafu Mali zote utazimiliki peke yako".
Lili kuwa wazo la Julieth kwa Mumewe japo Mumewe akulipokea kwa furaha lakini maneno matamu yaliyo toka katika kimya cha Julieth mkewe yalizidi kumshawishi hatimaye akakubali kumua Davi................
Itaendelea
Njoo WhatsApp 0747838773